Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.
Lakini mimi nikafikiri: Nimeshugulika bure, nimetumia nguvu zangu bure kabisa. Hata hivyo, Yawe atanipa haki yangu; mushahara wa kazi yangu uko kwa Mungu.
Mbona munatumia feza zenu kwa ajili ya kitu kisichokuwa chakula? Kwa nini kutoa jasho lenu kwa kitu kisichoshibisha? Munisikilize mimi kwa uangalifu, nanyi mutakula vinavyokuwa vitamu, na kufurahia vinavyokuwa bora.
Kama vile mbingu mupya na dunia mupya nitakazoumba zitakavyodumu milele kwa uwezo wangu, ndivyo wazao wako na jina lako litakavyodumu. –Ni ujumbe wa Yawe.–
Munapanda mbegu kwa wingi, lakini munavuna kidogo. Munakula, lakini hamushibi. Munakunywa divai, lakini hamutosheki. Munavaa nguo, lakini bado munasikia baridi. Mushahara wa mutumishi unakuwa kama umetumbukizwa katika mufuko uliotoboka.
Mulete katika gala yangu zaka yote, kusudi katika nyumba yangu kuwe chakula cha kutosha. Kisha munaweza kunijaribu. Munipime namna hiyo nanyi mutaona kama sitayafungua madirisha ya mbinguni na kuwatiririshia baraka tele.
Kwa hiyo ahadi inafuatana na imani, kusudi ikuwe imetolewa kwa neema ya Mungu. Na zaidi kuwe uhakikisho kwamba ahadi hiyo ni kwa ajili ya wazao wote wa Abrahamu, si kwa wale wanaotii Sheria tu, lakini vilevile kwa wale wanaokuwa na imani kama Abrahamu, babu yetu sisi wote.
Basi wandugu zangu wapenzi, musimame imara bila kutikisika. Muendelee kumutumikia Bwana siku zote, mukijua kwamba masumbuko munayopata kwa ajili ya Bwana hayatapita bure.