Nimeyaweka maneno yangu katika kinywa chako; nimekuficha katika kivuli cha mukono wangu. Mimi nilizitandaza mbingu, nikaiweka misingi ya dunia. Mimi ninawaambia, enyi watu wa Sayuni: Ninyi ni watu wangu.
Kama vile mbingu mupya na dunia mupya nitakazoumba zitakavyodumu milele kwa uwezo wangu, ndivyo wazao wako na jina lako litakavyodumu. –Ni ujumbe wa Yawe.–
Siku hizo, wakati mutakapokuwa mumeongezeka na kuwa wengi katika inchi, watu hawatalitajataja tena Sanduku langu la Agano. –Ni ujumbe wa Yawe.– Hawatalifikiri juu yake kabisa, wala hawatalikumbuka tena; hawatalihitaji, wala hawatatengeneza lingine.
Lakini ni kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Mambo yale ambayo hakuna mutu aliyepata kuyaona wala kuyasikia, mambo yale ambayo hakuna mutu aliyepata kufikiri juu yake, ndiyo yale Mungu aliyowatayarishia wale wanaomupenda.”