Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 65:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Watumishi wangu wataimba kwa furaha ndani ya moyo, lakini ninyi mutalia kwa uchungu ndani ya moyo na kupiga kelele kwa uchungu mukubwa ndani ya roho.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 65:14
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Waliokuwa karibu kuangamia walinitakia baraka. Niliwafanya wajane waone tena furaha ndani ya moyo.


Uwaache walaani, lakini wewe unibariki; wanaonishambulia wafezeheke, nami mutumishi wako nifurahi.


Dunia yote inakuabudu; watu wote wanakuimbia sifa!”


Mulie, maana siku ya Yawe imekaribia; inakuja kama uharibifu kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu.


Watu wanalalamika, wanaimba kwa shangwe. Kutoka upande wa magaribi, wanatangaza ukubwa wa Yawe,


Lakini ninyi munaowasha moto, na kujifanyia silaha za mienge, mutembee kwa mwangaza wa moto huo, ndimi za moto muliowasha ninyi wenyewe. Kitu mutakachopata kutoka kwa Yawe ni hiki: ninyi mutalala chini na mateso makali.


Watu wako uliowakomboa, ee Yawe, watarudia, watakuja Sayuni wakiimba; watajaa furaha ya milele, watapata furaha na shangwe. Huzuni na maombolezo vitatoweka kabisa.


Mutayaona hayo na mioyo yenu itafurahi; mifupa yenu itastawi tena kama vile majani mabichi. Kwa hiyo itajulikana kwamba mimi Yawe ninawalinda watumishi wangu, lakini nikikasirika ninawaazibu waadui zangu.


Maana miti mizito waliyobeba, nira walizokuwa wamefungwa, na fimbo ya wasimamizi, umezivunjavunja kama wakati wa Wamidiani.


Maana Yawe anasema hivi: Mushangilie kwa furaha kwa ajili ya Yakobo, mupige vigelegele kwa ajili ya taifa kubwa, mutangaze, musifu na kusema: Yawe ameokoa watu wake, ameleta ukombozi kwa wale waliobaki kati ya Waisraeli!


Nao watawatupa ndani ya furu la moto, na mule watalia na kusaga meno.


Halafu mufalme akawaambia watumishi wake: ‘Mumufunge mutu huyu miguu na mikono na kumutupa inje kwenye giza. Kule atalia na kusaga meno.’ ”


Lakini wale waliopaswa kushiriki katika Ufalme ule watatupwa inje kwenye giza, na kule watalia na kusaga meno.”


Na kule mutalia na kusaga meno, mutakapowaona Abrahamu, Isaka, Yakobo na manabii wote katika Ufalme wa Mungu. Lakini ninyi mutakuwa mumetupwa inje!


Basi, munisikilize sasa ninyi watajiri! Mulie na kuomboleza kwa sababu ya taabu itakayowapata.


Kati yenu kuna mutu anayekuwa katika mateso? Aombe kwa Mungu. Au kuna mutu anayekuwa katika furaha? Aimbe nyimbo za sifa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ