Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 65:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Nimewapangia kifo kwa upanga, ninyi wote mutanaswa kwa kuchinjwa! Maana, nilipowaita, hamukuniitikia; niliposema, hamukunisikiliza. Mulitenda maovu mbele yangu, mukachagua yale nisiyoyapenda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 65:12
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mujisafishe, mujitakase; muondoe matendo yenu maovu mbele yangu. Muache kutenda mabaya,


Lakini mukikataa na kuniasi, mutaangamizwa kwa upanga. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.


Hakuna! Mutajikunja tu kati ya wafungwa na kuangamia pamoja na wanaouawa katika vita. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Siku hiyo, Yawe atakamata upanga wake mukubwa, mukali na imara, na kuiazibu Leviatani, ile nyoka inayoruka na kuzongazonga. Yawe ataua nyoka mukubwa anayeishi katika bahari.


Wanaume wenu wataangamia kwa upanga, watu wenu wenye nguvu watakufa katika vita.


Yawe amekasirikia mataifa yote, amekasirikia majeshi yao yote. Ameyapangia mwisho wao, ameyatoa yaangamizwe.


Upanga wa Mungu uko tayari juu mbinguni. Angalia, unashuka kuwaazibu Waedomu, watu ambao ameamua kuwaangamiza.


Upanga utajaa damu na mafuta: damu ya kondoo na mbuzi, na mafuta ya figo za kondoo dume. Maana Yawe ana sadaka huko Bosira, kutakuwa mauaji makubwa katika inchi ya Edomu.


Nimeangalia vizuri sana, lakini simwoni mutu yeyote; hakuna yeyote kati ya hao miungu anayeweza kushauri; nikiuliza, hakuna anayeweza kunijibu.


Nilipokuja, kwa nini sikukuta mutu? Nilipoita mbona hamukuitikia? Mukono wangu ni mufupi hata nisiweze kuwaokoa ninyi? Sina nguvu ya kuwakomboa? Ninakausha bahari kwa kuikaripia, na mito ninaifanya kuwa jangwa; samaki wake wanakufa na kunuka kwa kukosa maji.


Ukweli umekosekana, naye anayeacha uovu ananyanganywa. Mungu aliona mambo hayo. Alichukizwa kwamba watu hawafuati sheria yake.


Kwa hasira yangu niliwaponda watu, niliwalewesha kwa kasirani yangu; damu yao niliimwanga chini.


Ni watu ambao wananichokoza waziwazi siku zote; wanatambikia miungu yao katika bustani, na kuifukizia ubani juu ya matofali.


Yawe atatoa hukumu kwa moto atawaazibu watu wote kwa upanga; nao atakaowaangamiza watakuwa wengi.


Maana, mimi ninayaona matendo yao yote, hakuna hata moja linalofichama mbele yangu. Maovu yao yote ni wazi mbele yangu.


Kwa hiyo uwaache watoto wao wakufe kwa njaa, uwaache wakufe kwa vita. Wake zao wakuwe tasa na wajane. Waume zao wakufe kwa magonjwa makali na vijana wao wachinjwe kwa upanga katika vita.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninyi hamukunitii juu ya kuwapatia wandugu zenu Waisraeli uhuru. Basi, nami vilevile nitawapatia ninyi uhuru: uhuru wa kuuawa kwa upanga katika vita, kuuawa kwa ugonjwa mukali na kwa njaa. Nitawafanya ninyi kuwa kitambulisho cha kuogopesha kwa falme zote katika dunia.


Kwa hiyo, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Ninawaletea Wayuda na wakaaji wote wa Yerusalema hasara zote nilizosema juu yao, kwa sababu mimi nilisema nao, lakini hawakunisikiliza; niliwaita, lakini hawakuniitikia.


Ninyi mumefanya mambo hayo yote. –Ni ujumbe wa Yawe.– Na hata niliposema nanyi tena na tena hamukunisikiliza. Nilipowaita hamukuitika.


Sasa wewe Yeremia utawaambia maneno haya yote, lakini wao hawatakusikiliza. Utawaita, lakini hawatakuitikia.


Nitawaletea upanga ambao utalipiza kisasi juu ya agano mulilovunja. Ninyi mutakimbilia katika miji yenu, lakini nitawaletea ugonjwa mukali na kuwatia katika mikono ya waadui zenu.


Haya ndiyo mambo ambayo mimi Yawe niliyowaambia kupitia kwa manabii wa zamani, wakati Yerusalema ulikuwa umestawi na wenye wakaaji tele, na wakati ambapo kulikuwa wakaaji wengi katika miji ya kandokando yake na katika eneo la Negebu na mabonde ya Sefela.


Yeye akawatuma watumishi wake kwa kuwaita watu wale walioalikwa kwa karamu, lakini hawakutaka kufika.


Halafu mufalme akakasirika. Akawatuma waaskari wake kuwaua wale wauaji na kuteketeza muji wao kwa moto.


Alikuja katika inchi yake, lakini taifa lake halikumupokea.


Vita itasababisha vifo vingi inje, na ndani ya nyumba hofu itawatawala. Vijana wanaume na wanawake watauawa, hata wenye kunyonya na wazee wenye imvi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ