Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 64:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Hakuna hata mumoja anayekuja kukuomba; hakuna anayejishugulisha kukutafuta. Wewe unauficha uso wako mbali nasi, umetuacha tufungwe na maovu yetu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 64:6
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wageni walivunjika moyo; wakakuja kutoka makimbilio yao wakitetemeka.


Nani anayeweza kutoa kitu kisafi kutoka kitu kichafu? Hakuna anayeweza.


Mutu anaweza basi namna gani kuwa mwenye haki mbele ya Mungu? Mwanadamu tu anaweza namna gani kujidai kuwa safi?


Mimi sifai kitu. Nitakujibu nini? Ninafunga kinywa changu.


Lakini waovu si vile hata kidogo. Wao ni kama maganda yanayopeperushwa na upepo.


Hao wanaotenda maovu hawajui kitu? Wanatafuna watu wangu kama mikate, wala hawajali Yawe.


Ninaitikia kabisa makosa yangu, siku zote ninaona waziwazi zambi yangu.


Lakini waasi na wenye zambi wote wataangamizwa pamoja; wanaomwacha Yawe watateketezwa.


Mutakuwa kama mialo ambayo majani yake yamekauka; kama shamba lisilokuwa na maji.


Lakini ewe taifa la Yakobo, haukuniabudu mimi; enyi watu wa Israeli, mulichoka nami!


Musikilize, enyi wenye vichwa vigumu, munisikilize enyi munaokuwa mbali na ukombozi.


Musikilize, enyi watu wa Yakobo, enyi munaojulikana kwa jina la Israeli, ninyi munaokuwa wa uzao wa Yuda. Ninyi munaapa kwa jina la Yawe, na kudai kwamba munamwabudu Mungu wa Israeli; lakini hayo si ukweli wala sawa.


Yawe anasema hivi: Kama nimeachana na mama yako Yerusalema, barua ya kuachana iko wapi? Nilikuwa na deni ya nani kwa kuwauzisha? Mukumbuke kwamba muliuzishwa kwa ajili ya maovu yenu, mama yenu alifukuzwa kwa ajili ya makosa yenu.


Nilipokuja, kwa nini sikukuta mutu? Nilipoita mbona hamukuitikia? Mukono wangu ni mufupi hata nisiweze kuwaokoa ninyi? Sina nguvu ya kuwakomboa? Ninakausha bahari kwa kuikaripia, na mito ninaifanya kuwa jangwa; samaki wake wanakufa na kunuka kwa kukosa maji.


Sisi wote tumepotea kama kondoo, kila mumoja wetu ameelekea njia yake. Lakini Yawe alimubebesha azabu, ambayo sisi wenyewe tuliistahili.


Basi, mimi nikasema: Ole kwangu! Mimi nimeangamia, maana, midomo yangu ni michafu, na watu ninaoishi nao ni wenye midomo michafu. Hata hivyo, kwa macho yangu mwenyewe, nimemwona Mufalme, Yawe wa majeshi.


Nitamungojea Yawe ambaye amejificha mbali na wazao wa Yakobo; nitamutumainia.


Umetuazibu kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, lakini mpaka sasa, ee Yawe, Mungu wetu, hatukuomba musamaha wako kwa kuziacha zambi zetu na kutambua uaminifu wako.


Basi, zoruba itawapeperusha, nao watapata haya kwa ajili ya sadaka zao.


Wote wamewaka hasira kama furu, na wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wao wote wameanguka, wala hakuna anayeniomba musaada.


Kama ukoma umemushika na umeenea mwili muzima, toka kwenye kichwa mpaka kwenye miguu kama vile kuhani atakavyoona,


Kuhani Mukubwa Yoshua alikuwa akisimama mbele ya malaika, akiwa amevaa nguo zenye kuchafuka.


Kwa maana ninajua kwamba hakuna kitu kizuri kinachokaa ndani yangu, ni kusema katika hali yangu ya kimwili. Ni hivi kwa sababu ninakuwa na utashi wa kufanya jambo jema, lakini sifikii kulifanya.


Ole kwangu, mimi mutu wa taabu! Ni nani atakayeniokoa kutoka katika mwili huu unaokuwa wa kufa?


na kuungana naye kabisa. Nami sihesabiwi haki tena kufuatana na mambo niliyofanya, ndiyo ile haki inayopatikana kwa njia ya kushika Sheria. Lakini ninahesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Kristo, ndiyo ile haki inatoka kwa Mungu, naye anamuhesabia haki yule anayeamini.


Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.


Halafu mumoja wa wale wazee akaniuliza: “Wale wanaovaa kanzu nyeupe ni watu gani nao wanatoka wapi?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ