Isaya 64:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Ingeteketea kama moto unavyochoma kichaka, kama vile moto unavyochemusha maji. Ukuje upate kuwajulisha waadui zako jina lako nayo mataifa yatetemeke mbele yako!
na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Utuchungulie kutoka mbinguni, ee Mungu, uone, utuangalie kutoka makao yako matakatifu na matukufu. Iko wapi bidii yako kwa ajili yetu na nguvu yako? Hatuoni tena upendo na huruma yako.
Tumekuwa kama watu ambao haujawatawala hata kidogo, kama watu ambao hawakujulikana kwa jina lako. Heri ungepasua mbingu ushuke chini, milima ingetetemeka mbele yako!
Siku zinakuja ambapo wakati wa kuvuna utafuata mbio wakati wa kulima, wakati wa kukamua zabibu utafuata mbio wakati wa kupanda mizabibu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Milima itabubujika divai mupya, navyo vilima vitatiririka divai.
Bwana wetu Yawe wa majeshi, anaigusa dunia nayo inatetemeka, na wakaaji wake wanaomboleza; dunia nzima inapanda na kushuka kama vile muto Nili wa Misri unavyojaa na kupunguka.
Siku hiyo, atasimama kwenye mulima wa Mizeituni unaokuwa upande wa mashariki wa Yerusalema. Mulima ule utagawanywa kwa sehemu mbili na bonde pana litatokea toka upande wa mashariki mpaka wa magaribi. Nusu moja itaelekea upande wa kaskazini na nusu ingine kusini.