Katika siku ya nane, Solomono aliwaaga watu; nao wakamutakia mufalme baraka, wakaenda kwao wakishangilia na kufurahi kwa sababu ya wema ambao Yawe aliuonyesha kwa Daudi, mutumishi wake, na kwa watu wake Waisraeli.
Siku iliyofuata ambayo ilikuwa siku ya makumi mbili na tatu ya mwezi wa saba, Solomono akawaaga watu waende kwao, wakishangilia na kufurahi ndani ya moyo kwa sababu ya mazuri ambayo Yawe alimutendea Daudi, Solomono na kwa watu wake Waisraeli.
Wakateka miji yenye kuta, wakatwaa inchi yenye utajiri, nyumba zenye vitu vingi vizuri, visima vilivyochimbwa, mashamba ya mizabibu na mizeituni pamoja na miti yenye matunda kwa wingi. Hivyo wakakula, wakashiba na kunenepa na kufurahia wema wako.
Hivyo, ukawatia katika mikono ya waadui zao, nao wakawatesa. Lakini wakiwa katika mateso yao, wakakulilia, nawe ukawasikiliza kutoka mbinguni. Na kwa rehema zako nyingi, ukawatumia viongozi wa kuwaokoa; nao wakawakomboa toka katika mikono yao.
Hawakukutumikia katika ufalme wao, wala walipofurahia mema yako mengi uliyowajalia kwa wingi, katika inchi kubwa na yenye mboleo uliyowapa hawakuyaacha matendo yao maovu.
Mukumbuke Abrahamu babu yenu, na Sara aliyewazaa ninyi. Abrahamu alikuwa hana mutoto wakati nilipomwita, lakini nilimubariki na kumufanya kuwa na wengi.
Basi ikiwa ninyi munaokuwa waovu munajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, zaidi sana Baba yenu anayekuwa mbinguni atawapa wale wanaomwomba vitu vizuri zaidi.