Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 63:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Nitakumbusha mema ya Yawe, sifa za Yawe, matendo yake yote kwetu, mambo mazuri aliyowatendea Waisraeli, rehema yake, na wingi wa wema wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 63:7
46 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika siku ya nane, Solomono aliwaaga watu; nao wakamutakia mufalme baraka, wakaenda kwao wakishangilia na kufurahi kwa sababu ya wema ambao Yawe aliuonyesha kwa Daudi, mutumishi wake, na kwa watu wake Waisraeli.


Siku iliyofuata ambayo ilikuwa siku ya makumi mbili na tatu ya mwezi wa saba, Solomono akawaaga watu waende kwao, wakishangilia na kufurahi ndani ya moyo kwa sababu ya mazuri ambayo Yawe alimutendea Daudi, Solomono na kwa watu wake Waisraeli.


Wakateka miji yenye kuta, wakatwaa inchi yenye utajiri, nyumba zenye vitu vingi vizuri, visima vilivyochimbwa, mashamba ya mizabibu na mizeituni pamoja na miti yenye matunda kwa wingi. Hivyo wakakula, wakashiba na kunenepa na kufurahia wema wako.


Hivyo, ukawatia katika mikono ya waadui zao, nao wakawatesa. Lakini wakiwa katika mateso yao, wakakulilia, nawe ukawasikiliza kutoka mbinguni. Na kwa rehema zako nyingi, ukawatumia viongozi wa kuwaokoa; nao wakawakomboa toka katika mikono yao.


Hata hivyo, kutokana na rehema zako nyingi, haukuwaachilia waangamie kabisa au kuwatupilia, maana wewe ni Mungu mwenye huruma na rehema.


Hawakukutumikia katika ufalme wao, wala walipofurahia mema yako mengi uliyowajalia kwa wingi, katika inchi kubwa na yenye mboleo uliyowapa hawakuyaacha matendo yao maovu.


Ee nafsi yangu, umusifu Yawe! Usisahau hata kidogo matendo mazuri yake yote.


Mumushukuru Yawe kwa wema wake na maajabu yake kwa wanadamu.


Mumushukuru Yawe kwa wema wake na maajabu yake kwa wanadamu.


Mumushukuru Yawe kwa wema wake na maajabu yake kwa wanadamu.


Mumushukuru Yawe kwa wema wake na maajabu yake kwa wanadamu.


Watatangaza sifa za uzuri wako mwingi, na kuimba juu ya haki yako.


Ee Yawe, ukumbuke rehema yako na wema wako ambazo ni za milele.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi inayoelekea wakati nabii Natani alipomufikia kwa kumwonya juu ya uzinzi alioufanya na Batiseba.


Nina hamu ya kukuona katika pahali pako patakatifu, nione nguvu yako na utukufu wako.


Lakini wewe, Bwana, ni Mungu wa rehema na huruma; wewe ni muvumilivu, mwingi wa wema na uaminifu.


Ee Bwana, wewe ni muzuri na mwenye kusamehe, mwingi wa wema kwa wote wanaokuomba.


Ni vizuri kukushukuru, ee Yawe, kuliimbia jina lako sifa, ee Mungu Mukubwa.


Yetro akafurahishwa na yote Yawe aliyotenda kwa ajili ya Waisraeli, kwa kuwaokoa toka katika mikono ya Wamisri.


Ee Yawe, Mungu wetu, tulipata kutawaliwa na wabwana wengine ambao si wewe, lakini tunakubali wewe pekee kuwa Mungu wetu.


Mukumbuke Abrahamu babu yenu, na Sara aliyewazaa ninyi. Abrahamu alikuwa hana mutoto wakati nilipomwita, lakini nilimubariki na kumufanya kuwa na wengi.


Milima inaweza kutoweka, vilima vinaweza kuondolewa, lakini rehema zangu kwako sitaziacha, agano langu la amani litaimarishwa. Ni Yawe anayekuhurumia anayesema hivyo.


Nilikuacha kwa muda mufupi tu. Kwa huruma nyingi, nitakurudisha.


Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa muda kidogo, lakini kwa wema wa milele nitakuonea huruma. Ni Yawe Mukombozi wako anayesema hivyo.


Waovu waache njia zao mbaya, watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya; wamurudilie Yawe apate kuwahurumia, wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.


Sisi wote tumekuwa kama watu wachafu; matendo yetu yote mema ni kama nguo chafu. Wote tunanyauka kama majani, uovu wetu unatupeperusha kama upepo.


Ingawa atatufanya tuhuzunike, atakuwa na huruma tena, kadiri ya wingi wa wema wake.


Maana, nitalifanya jina la Bali lisitajike tena katika kinywa chako.


Angalia jinsi gani uzuri na urembo wake unavyokuwa! Vijana wanaume na wanawake watastawi kwa wingi wa ngano na divai mupya.


Basi ikiwa ninyi munaokuwa waovu munajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, zaidi sana Baba yenu anayekuwa mbinguni atawapa wale wanaomwomba vitu vizuri zaidi.


Au haujali na uwingi wa wema, utulivu na uvumilivu wa Mungu? Haujui kwamba wema wake ungeweza kukuongoza hata upate kugeuka toka zambi?


Sheria ilitokea na kusababisha kuongezeka kwa makosa, lakini nafasi yoyote palipozidi zambi, neema ilizidi sana.


Lakini Mungu ni mwenye huruma nyingi. Alitupenda kwa upendo wake mukubwa;


Bwana wetu amenijalia neema kwa uwingi, amenipa imani na upendo tunaokuwa nao katika kuungana kwetu na Kristo Yesu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ