Kwa hiyo, nitawamwangia waadui zangu hasira yangu, nitawalipiza kisasi wapinzani wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–
Mupigie kelele za vita pande zote; sasa Babeli umejitoa ukamatwe. Vikingio vyote vimeanguka, kuta zake zimebomolewa. Ni malipizi ya Yawe. Basi muulipize kisasi. Muutendee kama vile ulivyotendea wengine.
Mukimbie kutoka Babeli, kila mutu apate kuyaokoa maisha yake! Musiangamizwe katika azabu yake, maana huu ndio wakati wa Mungu wa kulipiza kisasi, anaiazibu Babeli kama inavyostahili.
Nitawafanya watu wangu Waisraeli walipize kisasi juu ya Waedomu nao watawatendea Waedomu kadiri ya hasira na kasirani yangu. Halafu Waedomu watatambua uzito wa kisasi changu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
Na saa ile ile, kukatokea tetemeko kubwa la inchi, na sehemu moja ya kumi ya muji ikabomoka, na watu elfu saba wakakufa katika tetemeko lile. Watu waliobaki wakashikwa na hofu, nao wakamutukuza Mungu wa mbinguni.
Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!