Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 63:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, anayefika kutoka Bosira na nguo ya madoa mekundu? Ni nani huyo aliyevaa nguo ya utukufu, anatembea kwa nguvu zake kubwa? Ni mimi Yawe ninayetangaza ushindi wangu; nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 63:1
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Bela alipokufa, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosira akatawala pahali pake.


Atafunga punda wake katika muzabibu na mwana-punda wake kwenye muzabibu bora. Atafua nguo zake katika divai, na kanzu zake katika divai nyekundu.


Utupatie musaada juu ya waadui zetu, maana musaada wa mwanadamu haufai kitu.


Ee Yawe, usisahau mambo Waedomu waliyotenda, siku ile Yerusalema iliponyanganywa; kumbuka maneno haya waliyosema: “Mubomoe Yerusalema! Muongoe hata na misingi yake!”


Kwa matendo yako makubwa unatuitikia na kutuokoa, ewe Mungu mwokozi wetu. Wewe ndiwe tumaini la viumbe vyote katika dunia yote na mbali katika bahari.


Ni kitu gani kile kinachotoka katika jangwa kama munara wa moshi, kinachotoa harufu ya manemane na ubani, manukato yanayouzishwa na wachuuzi?


Ni nani huyu anayeonekana kama mapambazuko, muzuri kama mwezi, mwenye kungaa kama jua, na anatisha kama jeshi lenye bendera?


Ni nani huyu anayekuja kutoka katika jangwa, akimwegemea mupenzi wake? Mimi nilikuamusha chini ya muti wa mutofaa, pale ambapo mama yako aliona uchungu, pale ambapo mama yako alikuzaa.


Wote pamoja watashambulia Wafilistini wanaokuwa upande wa magaribi, pamoja watawanyanganya watu wanaokaa upande wa mashariki. Watawashinda Waedomu na Wamoabu, nao Waamoni watawatii.


Mujongee musikilize enyi mataifa, musikilize enyi watu. Sikiliza, ee dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, ulimwengu na vyote vinavyotoka humo!


Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


Hatavunja tete lililokunjama, hatazimisha utambi unaotoa moshi; ataimarisha sheria yangu kwa uaminifu.


Mimi sikusema kwa siri, wala katika inchi yenye giza. Mimi sikuwaambia wazao wa Yakobo wanitafute pahali kusipokuwa kitu. Mimi Yawe ninasema ukweli, maneno yangu ni ya kuaminika.


Mimi nimeapa kwa nafsi yangu, ninachosema ni ukweli, neno langu halitarudi nyuma: kila mwanadamu atanipigia magoti, kila mutu atafanya kiapo.


Maana mutoto amezaliwa kwa ajili yetu, tumepewa mutoto mwanaume. Naye atapewa mamlaka ya kutawala. Ataitwa: “Mushauri wa Ajabu”, “Mungu Mwenye Nguvu”, “Baba wa Milele”, “Mufalme wa Amani”.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Kerioti na Bosira. Kweli, hukumu imeifikia miji yote ya Moabu ya mbali na ya karibu.


Maana nimeapa kwa nafsi yangu kwamba muji wa Bosira utakuwa kitisho na mushangao, utakuwa uharibifu na kutumiwa kama mufano wa laana; vijiji vyote vitakuwa mabomoko siku zote. –Ni ujumbe wa Yawe.


Bwana wetu Yawe alisema hivi: Kwa sababu Waedomu wamefanya kisasi na Yuda, wakawalipiza watu wa Yuda kisasi kibaya sana


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wewe ndiwe niliyesema habari zako hapo zamani kwa njia ya watumishi wangu manabii wa Israeli, ambao walitabiri nyakati zile kwamba nitakuleta kusudi ushambulie watu wa Israeli.


Haya ni maono ya Obadia. Bwana wetu Yawe anasema hivi juu ya taifa la Edomu. Tumepata habari kutoka kwa Yawe; mujumbe ametumwa kati ya mataifa: Musimame! Tuende tupigane na taifa la Edomu!


Ewe muji wa Temani, mashujaa wako wataogopa na kila mutu juu ya mulima wa wazao wa Esau.


Yawe, Mungu wako, yuko pamoja nawe. Yeye ni shujaa anayekuletea ushindi. Yeye atakufurahia kwa furaha kubwa. Kwa upendo wake atakujalia uzima mupya. Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,


Yawe anasema hivi: Nimewapenda ninyi siku zote. Lakini ninyi wazao wa Yakobo munaniuliza: Umetupenda namna gani? Yawe anasema hivi: Si Esau alikuwa ndugu wa Yakobo? Hata hivyo nilimupenda Yakobo


Mungu si mutu, hata aseme uongo, wala si mwanadamu, hata abadilishe nia yake! Ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?


Yesu alipoingia Yerusalema, muji wote ukavuma. Watu wakaulizana: “Huyu ni nani?”


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


Ninyi ambao kwa imani munalindwa salama kwa nguvu za Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa kwa mwisho wa nyakati.


Alikuwa amevaa nguo iliyochovywa ndani ya damu. Jina lake ni: “Neno la Mungu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ