Isaya 62:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
8 Yawe ameapa kwa uwezo wake mukubwa, ameapa kwa nguvu yake akisema: Sitawapa tena waadui zako ngano yako; wala wageni hawatakunywa tena divai yako ambayo umeitoshea jasho.
Nitafanya kama nilivyofanya wakati wa Noa. Wakati ule niliapa kwamba sitaifunika tena dunia kwa mafuriko ya maji. Basi sasa ninaapa kwamba sitakukasirikia tena wala sitakukaripia tena.
Mbona munatumia feza zenu kwa ajili ya kitu kisichokuwa chakula? Kwa nini kutoa jasho lenu kwa kitu kisichoshibisha? Munisikilize mimi kwa uangalifu, nanyi mutakula vinavyokuwa vitamu, na kufurahia vinavyokuwa bora.
Watakula mazao yenu na chakula chenu; watawaua wana na wabinti zenu. Watachinja makundi yenu ya kondoo na ngombe; wataiharibu mizabibu yenu na miti yenu ya matunda ya tini. Miji yenu yenye kuzungukwa na kuta munayoitegemea, wataiharibu kwa silaha zao.
Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile nilipowachagua Waisraeli niliwaapia wazao wa Yakobo. Nilijijulisha kwao katika inchi ya Misri, nikawaapia nikisema: Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
basi, mimi nitafanya hivi: Nitawapiga kwa kuwaletea hofu kubwa ya rafla, kifua kikubwa na homa itakayowapofusha macho na kuwakondesha. Mutapanda mbegu zenu bila mafanikio maana waadui zenu ndio watakaozikula.
Nitarudisha hali ya mbele ya watu wangu Waisraeli. Watajenga miji yao iliyoharibiwa na kuishi ndani yake; watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima mashamba na kula mazao yake.
Ngombe wenu watachinjwa mbele ya macho yenu lakini hamutaonja hata kipande cha nyama yao. Punda wenu watatwaliwa kwa nguvu mbele ya macho yenu wala hamutarudishiwa. Kondoo wenu watapewa waadui zenu, na hakuna mutu atakayeweza kuwasaidia.