Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 62:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Juu ya kuta zako, ee Yerusalema, nimeweka walinzi, usiku na muchana hawatakaa kimya hata kidogo. Enyi munaomukumbusha Yawe ahadi yake, musikae kimya;

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 62:6
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninakuomba uniokoe sasa kutoka kwa ndugu yangu Esau, maana nina hofu kwamba atatushambulia na kutuua wote, mama pamoja na watoto.


Mutu yule alipoona kwamba hawezi kumushinda Yakobo, alimugusa Yakobo kwenye maunganio ya kiuno, naye akateguka alipokuwa anapigana naye.


Akifuata maagizo ya Daudi baba yake, alipanga zamu za kila siku za makuhani na za Walawi waliowasaidia makuhani kusifu na kutimiza kazi zao. Vilevile aliwapanga walinzi wa milango katika makundi aliyoweka kwa kulinda kila mulango; maana ndivyo Daudi, mutu wa Mungu alivyoamuru.


Ndani ya kuta zinazokuzunguka kuwe amani, nao usalama ukuwe ndani ya nyumba zako nzuri!”


Kumbuka, ee Yawe, mazarau ya waadui zako; taifa pumbafu linatukana jina lako.


Kumbuka taifa lako ulilojipatia tangia zamani, kabila ulilokomboa likuwe mali yako. Kumbuka mulima Sayuni pahali unapokaa.


Walinzi wa muji waliniona walipokuwa wanazunguka katika muji. Basi nikawauliza: Mumemwona mupenzi wangu wa moyo?


Walinzi wa muji walinikuta, walipokuwa wakizunguka katika muji. Wakanipiga na kuniumiza; nao walinzi wa mulango wakaninyanganya ushungi wangu.


Munikumbushe tena makosa yangu, tusambe nanyi, mutoe mashitaki yenu kusudi tuuone ukweli wenu!


Nimekuchora wewe katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako ninaziona mbele yangu siku zote.


Sikiliza sauti ya walinzi wako; wanaimba pamoja kwa furaha, maana wanaona kwa macho yao wenyewe kurudi kwa Yawe katika Sayuni.


Maana walinzi wa Israeli wote ni vipofu; wote hawana akili yoyote. Wote ni kama imbwa bubu wasioweza kufoka, wanalala tu na kuota ndoto, wanapenda sana kusinzia!


Kwa ajili ya Sayuni sitakaa kimya, kwa ajili ya Yerusalema sitatulia, mpaka kuokolewa kwake kuonekane kama umeme, wokovu wake utokee kama mwangaza.


Usitutupe, kwa ajili ya heshima ya jina lako; usikizarau kiti chako cha kifalme chenye utukufu. Ukumbuke agano ulilofanya nasi, wala usilivunje.


Kisha nikawawekea walinzi kwa kuwaarifu nikawaambia: Musikilize mulio wa baragamu. Lakini wao wakasema: Hatutausikiliza.


Ukumbuke, ee Yawe, mambo yaliyotupata! Utuangalie, uone haya yetu!


Sababu gani umetusahau kwa muda murefu hivyo na kutuacha siku nyingi hivyo?


Watu waliotangulia wakamukaripia na kumunyamazisha, lakini alizidi kulalamika, akisema: “Mwana wa Daudi, unisikilie huruma!”


Naye akaniambia: ‘Kornelio, Mungu amesikia maombi yako na kukukumbuka kwa ajili ya misaada unayotoa kwa wamasikini.


Kornelio akamukazia macho akiwa ameshikwa na woga, akamwuliza: “Bwana, ni nini?” Malaika akamujibu: “Mungu amesikia maombi yako na kupendezwa na misaada unayotoa kwa wamasikini, na kwa hiyo anakukumbuka.


Vilevile Mungu ameweka kwanza mitume katika kanisa; pili manabii na tatu walimu; kisha kunakuwa wale wenye zawadi ya kufanya miujiza, ya kuponyesha wagonjwa, ya kusaidia wengine, ya kuongoza wengine, ya kusema luga za ajabu.


Mutii waongozi wenu na kushika maagizo yao. Kwa maana wao wanashugulika kila mara kwa ajili ya roho zenu, na wao wanapaswa kutoa habari ya kazi yao mbele ya Mungu. Kwa kufanya vile mutawaruhusu kufanya kazi yao kwa furaha wala si kwa huzuni, kwa maana haitawafalia kitu kama wakitumika katika huzuni.


Watu wale wakalalamika hivi kwa sauti kubwa: “Bwana mutakatifu na mwenye ukweli, mpaka wakati gani utaendelea kungojea kuwahukumu wakaaji wa dunia na kuwaazibu kwa sababu ya kuuawa kwetu?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ