Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 62:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kwa ajili ya Sayuni sitakaa kimya, kwa ajili ya Yerusalema sitatulia, mpaka kuokolewa kwake kuonekane kama umeme, wokovu wake utokee kama mwangaza.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 62:1
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ulimi wangu ukuwe muzito, kama nisipokukumbuka wewe, ee Yerusalema, nisipokufurahia kuliko furaha yangu kubwa!


Kweli wewe haupendezwi na sadaka. Hautaki nikutolee sadaka za kuteketezwa.


Njia ya wenye haki ni kama mwangaza wa asubui mapema, ambao unaangaza zaidi na zaidi hata muchana kamili.


Mufungue milango ya muji, taifa aminifu liingie; taifa linalotenda mambo ya haki.


Siku ya kuwakomboa inakaribia, haiko mbali tena; siku ya kuwaokoa ninyi haitachelewa. Nitauokoa Sayuni, nitaleta utukufu kwa Israeli.


Ingekuwa heri ungalizitii amri zangu! Halafu baraka zingekutiririkia kama muto, ungefanikiwa kwa wingi kama mawimbi ya bahari.


Amuka! Amuka na nguvu, ee mukono wa Yawe! Amuka kama ulivyofanya hapo zamani, nyakati za vizazi vilivyopita. Si wewe ndiwe uliyemukatakata yule nyama mukubwa Rahabu, ukamutoboa yule nyoka mukubwa wa kuogopesha?


Yawe ameonyesha nguvu yake tukufu, mbele ya mataifa yote. Atawaokoa watu wake, na ulimwengu wote utashuhudia.


Utaimarishwa katika haki, mbali na kaoneo, nawe hautaogopa kitu; mbali na hofu, maana haitakukaribia.


Mukifanya hivyo mutaonekana kama mwangaza wa mapambazuko, na mutapona haraka. Matendo yenu mema yatawatangulia, nami nitawalinda kutoka nyuma kwa utukufu wangu.


Simama, ee Sayuni uangaze; maana mwangaza unatokea kwa ajili yako, utukufu wa Yawe unakuangazia.


Giza litaifunika dunia, giza kubwa litayafunika mataifa; lakini wewe, Yawe atakuangazia, utukufu wake utaonekana kwako.


Nao muji huu utakuwa kwangu jina la furaha, sifa na utukufu mbele ya mataifa yote katika dunia ambayo yatasikia juu ya mema yote ninayowafanyia. Mataifa yataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mema na amani nitakazouletea muji huu wa Yerusalema.


mataifa mengi yataufikia na kusema: Tuende juu kwenye mulima wa Yawe, tuende katika nyumba ya Mungu wa Yakobo, kusudi atufundishe njia zake, nasi tuzifuate. Maana sheria itatoka kule Sayuni; na neno la Yawe kule Yerusalema.


Yawe wa majeshi, ambaye kwa utukufu wake amenituma, anasema hivi juu ya mataifa yaliyowakamata mateka watu wake: Hakika, anayewagusa ninyi anagusa mboni ya jicho langu.


Vilevile, mwangaza wenu unapaswa kuangaza mbele ya watu, kusudi waone matendo yenu mazuri, nao wamutukuze Baba yenu anayekuwa mbinguni.


Akawaambia: “Mavuno ni mengi, lakini watumishi ni wachache. Basi muombe Bwana wa mavuno atume watumishi kwa kuyavuna.


Kwa mwisho wandugu, mutuombee, kusudi neno la Bwana lisambae upesi na kutukuzwa, kama vile inavyokuwa kwenu.


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ