Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 61:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kwa vile mulipata haya mara mbili, watu wakaona kwamba mazarau ni majaliwa yenu, sasa mutapata sehemu mara mbili kuwa mali yenu, na furaha yenu itadumu milele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 61:7
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walipofika ngambo, Elia akamwambia Elisha: “Uniambie jambo unalotaka nikufanyie mbele sijaondolewa kwako.” Elisha akamwambia: “Ninaomba sehemu mara mbili ya roho yako.”


Nyuma ya Yobu kuwaombea warafiki zake, Yawe akamurudishia Yobu hali yake ya kwanza. Akamupa mara mbili ya yote aliyokuwa nayo pale mbele.


Wanaopanda kwa machozi, watavuna kwa shangwe.


Unanionyesha njia ya kufikia uzima. Kuwa mbele yako ni kujazwa furaha, kuwa kwa kuume kwako kunapendeza milele.


Waliokombolewa na Yawe watarudi, watakuja Sayuni wakipiga vigelegele. Watakuwa wenye furaha ya milele, watajaliwa furaha na shangwe; huzuni na kilio vitatoweka kabisa.


Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.


Watu wako uliowakomboa, ee Yawe, watarudia, watakuja Sayuni wakiimba; watajaa furaha ya milele, watapata furaha na shangwe. Huzuni na maombolezo vitatoweka kabisa.


Usiogope, hautapata haya tena. Usifazaike, hautazarauliwa tena. Utaisahau haya uliyopata katika ujana wako, wala hautakumbuka tena mazarau ya ujane wako.


Wewe ulikuwa umeachwa na kuchukiwa, hakuna aliyependa hata kupita ndani yako. Lakini sasa nitakufanya ukuwe na utukufu milele, utakuwa muji wa furaha kwa kizazi na kizazi.


Watu wako wote watakuwa wa haki, nao watarizi inchi milele. Hao ni chipukizi nililopanda mimi, kazi ya mikono yangu kwa ajili ya utukufu wangu.


Basi, mimi Yawe ninasema: Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mutasikia njaa; watumishi wangu watakunywa, lakini ninyi mutasikia kiu; watumishi wangu watafurahi, lakini ninyi mutafezeheka.


Wakati huo, nitawaazibu wote wanaokugandamiza. Nitawaokoa vilema na kuwakusanya waliotupwa na kubadilisha haya yao kuwa sifa na utukufu katika dunia yote.


Sasa nitaleta tena amani katika dunia, mvua itanyesha kama kawaida, udongo utatoa mazao, na mizabibu itazaa kwa wingi. Nitawapa watu wanaobaki wa taifa hili yale yote yakuwe mali yao.


Enyi wafungwa wenye tumaini, murudi kwenye ukuta wa muji wenu. Sasa mimi ninawatangazia: nitawarudishia mema mara mbili.


Halafu hawa watakwenda kwenye nafasi watakapoazibiwa kwa milele, lakini wenye haki wataingia kwenye uzima wa milele.”


Kwa maana taabu tunayopata ni ndogo na ya muda tu, inatutayarishia utukufu mukubwa sana na wa milele unaokuwa muzuri zaidi kupita mateso haya.


Anapaswa kukubali yule muzaliwa wa kwanza, mutoto wa yule mwanamuke asiyependwa, na kumupa haki yake: sehemu ya mali zake mara mbili.


Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatufariji kwa milele na kutupatia tumaini njema,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ