Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 61:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Nanyi mutaitwa: “Makuhani wa Yawe”, Mutaitwa: “Watumishi wa Mungu wetu”. Mutafaidika kwa utajiri wa mataifa, mutatukuzwa kwa mali zao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 61:6
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Hayo ndiyo maneno utakayowaambia Waisraeli.”


Feza utakayopata itatakaswa kwa ajili ya Yawe. Hawatalinda feza hiyo lakini wale wanaomwabudu Yawe wataitumia kwa kununua chakula kingi na nguo nzuri.


maana utapanuka kila upande; wazao wako watarizi mataifa, miji iliyokuwa ukiwa itajaa watu.


Wageni watakaoshikamana nami Yawe, kwa kunitumikia na kwa kupenda jina langu, na kuwa watumishi wangu, wote watakaoshika siku ya Sabato bila kuichafua, watu watakaofuata agano langu,


Maana Yawe anasema hivi: Nitakuletea fanaka nyingi kama muto, utajiri wa mataifa kama muto uliofurika. Nanyi mutanyonya na kubebwa kama mutoto muchanga, mutabembelezwa kama mutoto juu ya magoti ya mama yake.


Vilevile nitawachagua wamoja kati yao kuwa makuhani na Walawi. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Vilevile nao makuhani wa ukoo wa Lawi watakuwa pale siku zote kwa kunitumikia wakinitolea sadaka za kuteketezwa na sadaka za unga na kunitolea sadaka milele.


Kwa hiyo Waisraeli hawataniacha tena na kujichafua wenyewe kwa kutenda zambi; kusudi wakuwe watu wangu nami nikuwe Mungu wao. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Basi wandugu zangu, kufuatana na vile Mungu alivyoonyesha huruma yake kwetu, ninawasihi mujitoe wenyewe kwake kuwa sadaka yenye uzima, takatifu na yenye kumupendeza. Hii ndiyo njia ya kweli ya kumwabudu.


Basi, Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi wa Mungu, waliowaonyesha ninyi njia ya kuamini. Tumefanya vile kila mumoja wetu kwa kadiri ya zawadi aliyopewa na Bwana.


Kwa hiyo mutuhesabu kama watumishi wa Kristo, wanaoshugulika na ujumbe wa siri wa Mungu.


Sasa nitasema kama mwenda-wazimu: wao ni watumishi wa Kristo? Mimi ni mutumishi wake zaidi kuliko wao. Nimetumika kazi nyingi zaidi, nimefungwa mara nyingi zaidi, nimepigwa zaidi, na mara nyingi nimekuwa katika hatari ya kufa.


Lakini tunaonyesha katika mambo yote kwamba sisi ni watumishi wa Mungu: tumedumu sana katika mateso, katika ukosefu na katika taabu.


Wala wasikuwe na urizi kati ya wandugu zao; Yawe ndiye urizi wao kama vile alivyoahidi.


Nanyi vilevile, kama mawe yenye uzima mutumiwe kwa kujenga hekalu la kiroho. Na mule mutafanya kazi takatifu ya ukuhani kwa kutoa sadaka za kiroho zinazomupendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


Hivi akatupatia ufalme wa kikuhani kusudi tumutumikie Mungu Baba yake. Yesu Kristo atukuzwe na kuwa na uwezo kwa milele na milele. Amina.


Heri na baraka sana kwa wale watakaokuwa katika ufufuko wa kwanza! Kifo cha pili hakina uwezo juu yao, nao watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, na watatawala pamoja naye kwa muda wa miaka elfu moja.


Umewapatia ufalme wa kikuhani kusudi wamutumikie Mungu wetu; nao watatawala katika dunia.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ