Kwa hiyo, nitawamwangia waadui zangu hasira yangu, nitawalipiza kisasi wapinzani wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–
Bwana wetu Yawe atakiangamiza kifo milele! Atayafuta machozi katika nyuso za watu wote na kuondoa haya ya watu wake katika dunia yote. Yawe amesema hivyo.
Yawe anasema hivi: Wakati uliofaa nilijibu maombi yako; wakati wa wokovu nilikusaidia. Nimekuweka na kukufanya ukuwe kiungo cha agano langu na mataifa yote: utatengeneza inchi na kurudisha tena inchi hiyo iliyoharibika.
Munapofunga kula, ninyi munajitaabisha; munaviinamisha vichwa vyenu kama utete, na kulalia nguo za magunia na majivu. Hii ndio munayoita mafungo ya kula chakula? Hiyo ni siku inayonipendeza mimi?
Mutayaona hayo na mioyo yenu itafurahi; mifupa yenu itastawi tena kama vile majani mabichi. Kwa hiyo itajulikana kwamba mimi Yawe ninawalinda watumishi wangu, lakini nikikasirika ninawaazibu waadui zangu.
Halafu wabinti zao watafurahi na kucheza, vijana na wazee watashangilia kwa furaha. Nitageuza maombolezo yao kuwa furaha, nitawafariji na kuwapa furaha pahali pa huzuni.
Lakini siku hiyo ni siku ya Bwana wetu Yawe wa majeshi. Ni siku ya kulipiza kisasi, siku ya kuwaazibu waadui zake. Upanga utawamaliza hao na kutosheka, utaikunywa damu yao na kushiba. Maana Bwana wetu Yawe wa majeshi yuko na sadaka huko kaskazini karibu na muto Furati.
Lakini kwa upande wangu, nimejazwa nguvu na roho ya Yawe; nimejaliwa kufuata sheria ya Mungu na kuwa na uwezo niwatangazie wazao wa Yakobo kosa lao, niwaambie Waisraeli zambi yao.
Kwa maana Mungu anasema hivi katika Maandiko Matakatifu: “Kwa wakati uliofaa, nilijibu maombi yako. Kwa siku ya wokovu, nilikusaidia.” Basi sasa, huu ndio wakati unaofaa, sasa leo ni siku ya wokovu.
Wanajikaza kutuzuiza tusitangaze Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kusudi wasiokoke. Hivi wanafikilia kwenye hatua ya mwisho ya zambi walizotenda siku zote. Lakini kwa mwisho kasirani ya Mungu imewaangukia.