Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 61:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Nitafurahi sana kwa sababu ya Yawe, nafsi yangu itashangilia kwa sababu ya Mungu wangu. Maana amenivalisha nguo ya wokovu, amenifunika kanzu ya haki, kama bwana arusi anavyojipamba kwa shada la maua, kama bibi arusi anavyojipamba kwa ushanga wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 61:10
52 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha akatoa vyombo vya feza na zahabu na nguo, akamupa Rebeka. Vilevile aliwapa wandugu na mama ya Rebeka mapambo ya bei kubwa.


“Sasa, ee Yawe, Mungu, uingie pahali pako pa kupumzika, wewe pamoja na Sanduku la Agano la nguvu zako. “Ee Yawe, Mungu, makuhani wako wapate wokovu, na watakatifu wako wafurahie uzuri wako.


Sasa murudi kwa nyumba mufanye sherehe, mukule vyakula na kunywa divai nzuri, lakini mukumbuke kuwapelekea wale ambao hawana kitu cha kutosha; maana leo ni siku takatifu kwa Bwana wetu. Musihuzunike kwa sababu furaha Yawe anayowajalia itawapa nguvu.”


Haki ilikuwa ndiyo nguo yangu; kufuata sheria ya Mungu kulikuwa kama vile kanzu na taji langu.


Nitawavalisha makuhani wake katika wokovu, waaminifu wake watapiga vigelegele vya furaha.


Makuhani wako wakuwe watu wa haki siku zote; na waaminifu wako wapige vigelegele vya furaha!


Yawe ndiye nguvu na ngao yangu; tegemeo la moyo wangu ni kwake. Amenisaidia, nami nikashangilia kwa moyo wote; kwa wimbo wangu ninamushukuru.


Hivi nitamufurahia Yawe; nitashangilia kwa sababu yeye ameniokoa.


Pete za masikio zinapendeza mashavu yako. Mikufu ya mawe ya bei kali inapendeza shingo yako.


Siku hiyo mutasema: Ninakushukuru, ee Yawe, maana ingawa ulinikasirikia, hasira yako imetoweka, nawe umenifariji.


Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.


Maana wewe Israeli umemusahau Mungu aliyekuokoa, haukukumbuka Jiwe lako la kufichamia. Kwa hiyo, hata mukipanda mimea ya Bali, na kuitakasa kwa mungu wa kigeni;


Wewe, ee Yawe, ndiwe Mungu wangu; nitakutukuza na kulisifu jina lako, kwa maana umetenda mambo ya ajabu; unaitimiza kwa uaminifu na kweli mipango uliyoipanga tangu zamani.


Siku ile, watu wote watasema: Huyu ndiye Mungu wetu! Tumemungojea atuokoe. Huyu ndiye Yawe tuliyemutazamia. Mukuje tufurahi na kushangilia kwa sababu ametuokoa.


Waliokombolewa na Yawe watarudi, watakuja Sayuni wakipiga vigelegele. Watakuwa wenye furaha ya milele, watajaliwa furaha na shangwe; huzuni na kilio vitatoweka kabisa.


Mutaipepeta milima hiyo, nao upepo utaipeperushia mbali, zoruba itaitawanya huko na huko. Nanyi mutafurahi kwa sababu yangu Yawe; mutaona utukufu kwa sababu yangu Mungu Mutakatifu wa Israeli.


Ingekuwa heri ungalizitii amri zangu! Halafu baraka zingekutiririkia kama muto, ungefanikiwa kwa wingi kama mawimbi ya bahari.


Inua macho uangalie pande zote; watu wako wote wanakusanyika na kukufikia. Kama vile ninavyoishi, watu wako watakuwa kwako kama mapambo, utawafurahia kama vile bibi arusi anavyofanya na taji lake. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini mimi nikafikiri: Nimeshugulika bure, nimetumia nguvu zangu bure kabisa. Hata hivyo, Yawe atanipa haki yangu; mushahara wa kazi yangu uko kwa Mungu.


Watu wako uliowakomboa, ee Yawe, watarudia, watakuja Sayuni wakiimba; watajaa furaha ya milele, watapata furaha na shangwe. Huzuni na maombolezo vitatoweka kabisa.


Mimi Yawe nitaufariji Sayuni, nitatengeneza pahali pake pote palipoharibika. Nitazifanya mbuga zake kama shamba la Edeni, jangwa yake kama bustani ya Yawe. Ndani yake kutapatikana furaha na shangwe, na nyimbo za shukrani zitasikilika humo.


Amuka! Amuka! Ujipatie zile nguvu zako, ewe Sayuni! Uvae nguo yako nzuri, ewe Yerusalema, muji mutakatifu. Maana hawataingia tena kwako watu wasiotahiriwa na wachafu.


hao nitawaleta katika mulima wangu mutakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya maombi; sadaka zao na sadaka za kuteketezwa zitakubaliwa kwenye mazabahu yangu. Maana nyumba yangu itaitwa: Nyumba ya maombi kwa ajili ya watu wote.


utapata furaha yako kwangu mimi Yawe, nitakupatia ushindi katika kila upinzani katika inchi, nitakulisha mali ya Yakobo, babu yako. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.


na kuwapa wale wanaoomboleza katika Sayuni taji la maua pahali pa majivu juu ya kichwa, mafuta ya kuangarisha kwa furaha pahali pa maombolezo, nguo ya sifa pahali pa moyo muzito. Nao wataitwa miti ya mialo ya haki, Yawe aliyopanda kuonyesha utukufu wake.


Mufurahi na kushangilia milele, kwa ajili ya vitu hivi ninavyoumba. Yerusalema nitaifanya muji wa shangwe, na watu wake watu wenye furaha.


Kijana binti anaweza kusahau mapambo yake, au bibi arusi nguo yake? Lakini watu wangu wamenisahau kwa muda wa siku zisizohesabika.


Makuhani ambao watakuwa wakitumika katika Pahali Patakatifu, wanapotaka kwenda kwenye kiwanja cha inje, ni lazima waache humo nguo zao walizovaa walipokuwa wanatumika mbele ya Yawe kwa sababu nguo hizo ni takatifu. Ni lazima wavae nguo zingine mbele ya kutoka inje ambako watu wanakusanyika.


mimi nitaendelea kumufurahia Yawe. Nitamushangilia Mungu anayeniokoa.


Watu wa Efuraimu watakuwa kama mashujaa katika vita; watajaa furaha kama watu waliokunywa divai. Watoto wao wataona hayo na kufurahi, watajaa furaha ndani ya moyo kwa sababu yangu mimi Yawe.


Kisha akawaambia wamuvalishe kitambaa safi juu ya kichwa. Hivyo, wakamuvalisha kitambaa safi na nguo; naye malaika wa Yawe alikuwa akisimama pale.


Lakini baba yake akawaambia watumishi wake: ‘Mulete mbio kanzu nzuri sana na kumuvalisha nayo. Mumuvalishe pete kwenye kidole chake na mumuvalishe viatu.


Lakini Bwana Yesu akuwe kama vile silaha munayobeba, musijiachilie kuvutwa na hali yenu ya kimwili hata mutimize tamaa zake.


Kwa maana kazi ya Ufalme wa Mungu si kushugulika na mambo ya kula na kunywa, lakini ni kushugulika na haki, amani na furaha vinavyotolewa na Roho Mutakatifu.


kuhesabiwa haki na Mungu kunapatikana kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote wanaoamini, kwa maana hakuna tofauti yoyote kati yao,


Wala si ile tu, lakini tunafurahi kwa ajili ya Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo aliyetupatanisha sasa na Mungu.


Hivi, ninyi wote mulioungana na Yesu Kristo, kwa njia ya kubatizwa, ni kama vile mumevaa Kristo.


na kuungana naye kabisa. Nami sihesabiwi haki tena kufuatana na mambo niliyofanya, ndiyo ile haki inayopatikana kwa njia ya kushika Sheria. Lakini ninahesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Kristo, ndiyo ile haki inatoka kwa Mungu, naye anamuhesabia haki yule anayeamini.


Mufurahi siku zote katika kuungana kwenu na Bwana. Na tena ninasema: Mufurahi!


Ninyi munamupenda ijapokuwa hamujamwona, na munamwamini ijapokuwa sasa hamumwoni. Na zaidi ya ile munashangilia kwa furaha isiyoweza kuelezwa, inayojaa utukufu,


Nikaona muji mutakatifu, ndio Yerusalema mupya, uliokuwa ukishuka toka mbinguni kwa Mungu, nao ukitengenezwa vizuri kama vile bibi arusi aliyepambwa kwa ajili ya kwenda kukutana na mume wake.


Kisha mumoja wa wale wamalaika saba walioshika vile vikombe vilivyojaa mapigo saba ya mwisho, akajongea na kuniambia: “Kuja nitakuonyesha bibi arusi, muke wa Mwana-Kondoo.”


Na kiti kile kilikuwa kimezungukwa na viti vingine makumi mbili na vine vya kifalme na juu ya viti vile kulikuwa kumeikaa wazee makumi mbili na wane. Wale wazee walikuwa wamevaa nguo nyeupe na juu ya kichwa chao kulikuwa taji za zahabu.


Halafu Hana aliomba na kusema: Ninamushangilia Yawe ndani ya moyo wangu. Ninamutukuza Yawe anayekuwa nguvu yangu. Ninawachekelea waadui zangu; maana ninaufurahia wokovu wako.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ