Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 60:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Makundi ya nyama wa inchi ya Kedari yatakusanyika kwako, utaweza kuwatumia kondoo dume wa Nebayoti; utatoa sadaka inayokubaliwa kwenye mazabahu ya Mungu, naye ataitukuza nyumba yake tukufu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 60:7
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Haya ni majina yao kufuatana na kuzaliwa kwao: Nebayoti, muzaliwa wa kwanza, Kedari, Adibeli, Mibusamu,


Kwa hiyo mutwae ngombe dume saba na kondoo dume saba, muende kwa mutumishi wangu Yobu, mutoe nyama wale kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Naye mutumishi wangu Yobu atawaombea, nami nitaisikiliza maombi yake na kuacha kuwatendea kulingana na upumbafu wenu; maana hamukusema ukweli juu yangu kama mutumishi wangu Yobu alivyofanya.”


Ole wangu maana ninaishi kama mugeni huko Meseki; ninaishi kama mugeni katika mahema ya Kedari.


Enyi wabinti wa Yerusalema, mimi ni mweusi. Ninapendeza kama mahema ya Kedari, kama mapazia ya nyumba ya Solomono.


Siku hiyo, kutakuwa mazabahu kwa ajili ya Yawe katikati ya inchi ya Misri, na nguzo iliyotakaswa kwa ajili ya Mungu kwenye mpaka wa Misri.


Yawe atajijulisha kwa Wamisri na hapo ndipo Wamisri watakapomwitikia na kumwabudu kwa kumutolea matoleo na sadaka za kuteketezwa. Vilevile watafanyia Yawe viapo ambavyo watavitimiza.


Maana Bwana aliniambia hivi: Katika muda wa mwaka mumoja, bila kuzidi wala kupunguka, utukufu wote wa Kedari utakwisha.


jangwa na miji yake yote vipige kelele, vijiji vya wakaaji wa Kedari vimusifu, wakaaji wa Sela waimbe kwa shangwe; wapige kelele kutoka juu kwenye mulima.


hao nitawaleta katika mulima wangu mutakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya maombi; sadaka zao na sadaka za kuteketezwa zitakubaliwa kwenye mazabahu yangu. Maana nyumba yangu itaitwa: Nyumba ya maombi kwa ajili ya watu wote.


Utaletewa utukufu wa pori ya Lebanoni: mbao za shindano, mivinje na misunobari, zitumike kwa kupamba kiwanja cha hekalu langu; nami nitaleta utukufu hapo ninapokaa.


Maana, katika mulima wangu mutakatifu, mulima murefu wa Israeli, ninyi wote watu wa Israeli mutanitumikia kule. –Ni ujumbe wa Yawe.– Huko mimi nitawapokea na kungojea muniletee sadaka na matoleo yenu bora na matoleo iliyotakaswa.


Waarabu na wakubwa wote wa inchi ya Kedari walikuwa wachuuzi wako wakubwa katika biashara ya wana-kondoo, kondoo dume na mbuzi.


Kutakuja wakati ambapo mulima wa nyumba ya Yawe utakuwa mukubwa kuliko milima yote. Utanyanyuliwa juu ya vilima vyote. Watu wengi watakimbilia kule,


Kutoka ngambo ya mito ya Kushi watu wangu wanaoniomba, wale ambao wametawanyika, wataniletea sadaka yangu.


Basi, huyo malaika aliyezungumuza nami akamwambia yule mwenzake: Kimbia umwambie yule kijana kwamba si lazima Yerusalema ukuwe na kuta, kama sivyo hapatakuwa nafasi ya kuwatoshelea wakaaji wake wengi na nyama watakaokuwa ndani yake.


Basi wandugu zangu, kufuatana na vile Mungu alivyoonyesha huruma yake kwetu, ninawasihi mujitoe wenyewe kwake kuwa sadaka yenye uzima, takatifu na yenye kumupendeza. Hii ndiyo njia ya kweli ya kumwabudu.


kuwa mutumishi wa Yesu Kristo kwa watu wa mataifa mengine. Ninafanya kazi ya ukuhani ya kuhubiri Habari Njema ya Mungu, kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuwa kama sadaka inayokubaliwa na Mungu na iliyotakaswa na Roho Mutakatifu.


Sisi tuko na mazabahu yetu, nao makuhani Wayuda wanaotumika katika Pahali Patakatifu hawana ruhusa ya kula sehemu ya vitu vinavyotolewa sadaka juu ya mazabahu ile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ