Isaya 60:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
5 Halafu utaona na utafurahi, moyo wako utasisimuka na kushangilia. Maana utajiri tokea ngambo ya bahari utakufikia kwa wingi, mali za mataifa zitaletwa kwako.
Maana Yawe anasema hivi: Nitakuletea fanaka nyingi kama muto, utajiri wa mataifa kama muto uliofurika. Nanyi mutanyonya na kubebwa kama mutoto muchanga, mutabembelezwa kama mutoto juu ya magoti ya mama yake.
Nao muji huu utakuwa kwangu jina la furaha, sifa na utukufu mbele ya mataifa yote katika dunia ambayo yatasikia juu ya mema yote ninayowafanyia. Mataifa yataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mema na amani nitakazouletea muji huu wa Yerusalema.
Nyuma, Waisraeli watarudi na kumutafuta Yawe, Mungu wao, na kumutafuta mufalme wao, wa uzao wa Daudi. Halafu watamutii Yawe, na kutazamia wema wake siku za mwisho.
Na wale wanafunzi Wayuda waliofika pamoja na Petro wakashangaa sana kwa kuona kwamba Mungu ametoa zawadi ya Roho wake Mutakatifu kwa watu wa mataifa mengine vilevile.
Basi ikiwa Mungu aliwapa wale watu zawadi ile ile Roho Mutakatifu aliyotupatia sisi wakati tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani hata nisubutu kupingana na Mungu?”
Wandugu zangu, sitaki mukose kujua siri hii, kusudi musijione kuwa wenye akili sana. Siri ile ni hii: Waisraeli wamoja wataendelea kuwa wagumu mpaka watu wa mataifa mengine kwa jumla watakapokuja kwa Mungu.
Basi, hatujivuni kupita kipimo juu ya kazi ya watu wengine. Lakini tunatumaini kwamba imani yenu itakapokuwa ikiongezeka, tutaweza kufanya kazi kubwa zaidi kati yenu kufuatana na kipimo cha kazi tuliyopewa na Mungu.
Watawaalika wageni kwenye milima yao, na huko watu watatolea sadaka. Maana wao watapata utajiri wao kutoka katika bahari na hazina zao katika muchanga wa pembeni ya bahari.”
Halafu Hana aliomba na kusema: Ninamushangilia Yawe ndani ya moyo wangu. Ninamutukuza Yawe anayekuwa nguvu yangu. Ninawachekelea waadui zangu; maana ninaufurahia wokovu wako.