Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 60:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Utaletewa chakula na watu wa mataifa; wafalme watakupatia chakula bora. Hapo utatambua kwamba mimi Yawe ni Mwokozi wako; mimi Mwenye Nguvu wa Yakobo ni Mukombozi wako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 60:16
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitawafanya kuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. Ninyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika nira za Wamisri.


Kwa hiyo, nitawamwangia waadui zangu hasira yangu, nitawalipiza kisasi wapinzani wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–


Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.


Mazabahu hayo yatakuwa kitambulisho na ushuhuda kwa Yawe wa majeshi katika inchi ya Misri. Watu wakimulilia Yawe humo kwa sababu ya kugandamizwa, yeye atawapelekea mukombozi atakayewatetea na kuwakomboa.


Siku ile, watu wote watasema: Huyu ndiye Mungu wetu! Tumemungojea atuokoe. Huyu ndiye Yawe tuliyemutazamia. Mukuje tufurahi na kushangilia kwa sababu ametuokoa.


Waliopotoka katika roho watapata maarifa na wenye kunungunika watakubali kufundishwa.


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


Mimi peke yangu ndiye Yawe, hakuna mukombozi mwingine isipokuwa mimi.


Kweli wewe ni Mungu mwenye kufichama, Mungu wa Israeli, Mungu mwokozi.


Mutangaze na kusema habari zenu. Mufanye shauri pamoja! Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa? Ni nani aliyesema mambo haya zamani? Haikukuwa mimi Yawe? Hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi! Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi; hakuna mwingine isipokuwa mimi.


Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Nitawasukuma watesaji wako wakule miili yao wenyewe; watalewa damu yao wenyewe kama divai. Halafu wanadamu wote watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mwokozi wako, Mukombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.


Kwa hiyo watu wangu watajua mimi ni nani. Siku hiyo watajua kwamba ni mimi ninayesema: “Niko!”


Naye atakuja katika Sayuni kama Mukombozi, Mukombozi wa wazao wa Yakobo ambao wataachana na makosa yao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Pahali pa shaba nitakuletea zahabu, pahali pa chuma nitakuletea feza, pahali pa miti, nitakuletea shaba, na pahali pa mawe nitakuletea chuma. Amani itatawala juu yako, haki itakuongoza.


Nanyi mutaitwa: “Makuhani wa Yawe”, Mutaitwa: “Watumishi wa Mungu wetu”. Mutafaidika kwa utajiri wa mataifa, mutatukuzwa kwa mali zao.


Maana wewe ndiwe Baba yetu; Abrahamu, babu yetu, hatujali, naye Israeli hatutambui; lakini wewe, ee Yawe, ni Baba yetu. Wewe umeitwa tangu zamani: Mukombozi wetu.


Maana alisema juu yao: Hakika, hawa ni watu wangu; watoto wangu ambao hawatanidanganya. Basi yeye akakuwa Mwokozi wao.


Mutayaona hayo na mioyo yenu itafurahi; mifupa yenu itastawi tena kama vile majani mabichi. Kwa hiyo itajulikana kwamba mimi Yawe ninawalinda watumishi wangu, lakini nikikasirika ninawaazibu waadui zangu.


Nitakuokoa toka katika mikono ya watu waovu, na kukuopoa toka katika makucha ya watesaji.


Nao watajua kwamba mimi Yawe, Mungu wao, niko pamoja nao na kwamba watu hao wa inchi ya Israeli ni watu wangu.


Kwa hiyo watu wa mataifa watatembea katika mwangaza wake na wafalme wa dunia wataleta utajiri wao ndani yake.


Heshima na utukufu za watu wote wa mataifa zitaletwa ndani ya muji ule.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ