Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 60:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Yawe anasema: Wageni watazijenga upya kuta zako, wafalme wao watakutumikia. Maana kwa hasira yangu nilikupiga, lakini kwa wema wangu nimekuhurumia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 60:10
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wewe, ee Yawe, unatawala milele; jina lako linakumbukwa katika vizazi vyote.


Mumwimbie Yawe sifa, enyi waaminifu wake; mukumbuke utakatifu wake na kumushukuru.


Siku hiyo mutasema: Ninakushukuru, ee Yawe, maana ingawa ulinikasirikia, hasira yako imetoweka, nawe umenifariji.


Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Wageni watakaoshikamana nami Yawe, kwa kunitumikia na kwa kupenda jina langu, na kuwa watumishi wangu, wote watakaoshika siku ya Sabato bila kuichafua, watu watakaofuata agano langu,


Mataifa watatembea katika mwangaza wako, wafalme watavutwa na kungaa kwako.


Amenituma kutangaza mwaka wake wa neema, na siku ya Mungu wetu ya kulipiza kisasi kusudi niwafariji wote wanaoomboleza.


Wageni watakuwa hapo kuwachungia makundi yenu ya nyama; watawalimia na kuwatunzia mizabibu yenu.


Miji yako mitakatifu imekuwa jangwa; Sayuni umekuwa matongo, Yerusalema umekuwa uharibifu.


Vilevile nitawachagua wamoja kati yao kuwa makuhani na Walawi. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Yawe anaipenda inchi yake anawahurumia watu wake.


Watu wanaokaa katika inchi za mbali watakuja kusaidia kwa kulijenga hekalu langu mimi Yawe. Nanyi mutajua kwamba Yawe wa majeshi, ndiye aliyenituma kwenu. Haya yote yatatukia kama mukiitii sauti ya Yawe, Mungu wenu.


Kwa hiyo watu wa mataifa watatembea katika mwangaza wake na wafalme wa dunia wataleta utajiri wao ndani yake.


Heshima na utukufu za watu wote wa mataifa zitaletwa ndani ya muji ule.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ