Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 60:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Simama, ee Sayuni uangaze; maana mwangaza unatokea kwa ajili yako, utukufu wa Yawe unakuangazia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 60:1
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mataifa yataheshimu jina la Yawe; wafalme wote katika dunia wataogopa utukufu wake.


Ee muji wa Mungu, mambo ya utukufu yanasemwa juu yako.


Sasa, enyi wazao wa Yakobo, mukuje, tutembee katika mwangaza wa Yawe.


Kisha mwezi utafezeheka, nalo jua litapata haya ya kuangaza, maana Yawe wa majeshi atatawala kule Yerusalema katika mulima Sayuni; ataonyesha wazee wa watu wake utukufu wake.


Siku ile Yawe wa majeshi atakuwa taji tukufu, kama kitambaa kizuri kwa watu wake watakaobaki wazima.


Litachanua maua kwa wingi kama waridi, litashangilia na kuimba kwa furaha. Mungu atalijalia utukufu wa milima ya Lebanoni, uzuri wa mulima Karmeli na wa bonde la Saroni. Watu watauona utukufu wa Yawe, watauona ukubwa wa Mungu wetu.


Halafu, kila pahali juu ya mulima Sayuni na juu ya mikutano ya watu atafanya kuwe wingu wakati wa muchana, na moshi na moto unaowaka vizuri wakati wa usiku. Zaidi ya hayo utukufu wa Mungu utaufunika na kuulinda muji wote.


Mimi Yawe nimekuita kutenda haki, nimekushika mukono na kukulinda. Kwa njia yako nitafanya ahadi na watu wote, wewe utakuwa mwangaza wa mataifa.


Mukifanya hivyo mutaonekana kama mwangaza wa mapambazuko, na mutapona haraka. Matendo yenu mema yatawatangulia, nami nitawalinda kutoka nyuma kwa utukufu wangu.


Kwa ajili ya Sayuni sitakaa kimya, kwa ajili ya Yerusalema sitatulia, mpaka kuokolewa kwake kuonekane kama umeme, wokovu wake utokee kama mwangaza.


Mataifa watauona wokovu wako, wafalme wote watauona utukufu wako. Nawe utaitwa kwa jina jipya ambalo litapangwa na Yawe mwenyewe.


Hivi mutapata kunyonya, nanyi mutashiba kwa riziki zake; mutayakunywa na kufurahi, kutokana na wingi wa utukufu wake.


Wewe, ee Mungu, umeongoza taifa, umezidisha furaha yake. Watu wanafurahi mbele yako wana furaha kama kwa wakati wa mavuno, kama vile wanaogawanya vitu walivyonyanganya wanavyofurahi.


Nao utukufu wa Yawe uliingia katika nyumba ya Yawe kwa njia ya mulango wa mashariki.


Watu hao wanaokaa katika giza, mwangaza umewatokea! Hao wanaoishi katika inchi yenye giza nzito sana ya lufu, wameona mwangaza mukubwa.”


Vilevile, mwangaza wenu unapaswa kuangaza mbele ya watu, kusudi waone matendo yenu mazuri, nao wamutukuze Baba yenu anayekuwa mbinguni.


Ndio utakaowaangazia mataifa, na kuleta utukufu kwa watu wako Waisraeli.”


Ule mwangaza wa kweli, unaomwangazia kila mutu, unakuja katika dunia.


Mimi nimekuja katika dunia kama mwangaza, kusudi mutu yeyote anayeniamini asikae katika giza.


Hukumu inatokana na hivi: mwangaza umekuja katika ulimwengu, lakini watu wanapenda giza kuliko mwangaza, kwa sababu matendo yao ni mabaya.


Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ni mwangaza wa dunia. Yeye anayenifuata hatatembea katika giza hata kidogo, lakini atakuwa na mwangaza wa uzima.”


Kwa maana yote yanayoonekana wazi yanageuka mwangaza. Ni kwa hiyo inasemwa hivi: “Amuka wewe unayelala! Ufufuke kutoka kati ya wafu, naye Kristo atakuangazia.”


Zamani muliishi katika giza, lakini sasa, kwa kuungana kwenu na Bwana, munaishi katika mwangaza. Muishi kama watoto wa mwangaza,


kusudi mupate kuwa bila kosa na kuwa na maisha safi. Hivi mutakuwa watoto wakamilifu wa Mungu wasiokuwa na kilema kati ya watu waovu na wapotovu wa dunia hii. Munapaswa kuangaza kati ya watu hawa kama vile nyota zinavyoangaza katika mbingu,


Ninyi ni wenye heri kama watu wakiwatukana kwa ajili ya Kristo, kwa kuwa Roho wa utukufu, maana yake Roho wa Mungu anakaa ndani yenu.


nao ukingaa kwa utukufu wa Mungu. Mwangaza wake ulikuwa kama jiwe la bei kali la yaspi, linalongaa kama kioo.


Muji ule hauna lazima ya mwangaza wa jua, wala wa mwezi, kwa sababu utukufu wa Mungu unauangazia na Mwana-Kondoo ndiye taa yake.


Hakutakuwa usiku tena, wala hawatakuwa na lazima ya mwangaza wa taa wala jua, kwa sababu Bwana wetu na Mungu wetu mwenyewe atawaangazia, nao watatawala milele na milele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ