Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 6:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Basi, mimi nikasema: Ole kwangu! Mimi nimeangamia, maana, midomo yangu ni michafu, na watu ninaoishi nao ni wenye midomo michafu. Hata hivyo, kwa macho yangu mwenyewe, nimemwona Mufalme, Yawe wa majeshi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 6:5
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yakobo akaita pahali pale Penueli, akisema: “Nimemwona Mungu uso kwa uso, nami sikukufa.”


Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu? Ni Yawe, wa majeshi, yeye ndiye Mufalme mwenye utukufu.


wakamwona Mungu wa Israeli. Chini ya miguu yake kulikuwa kitu kama sakafu ya mawe ya yakuti samawi, kikiwa safi kama mbingu inayoangaa.


Kisha Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.” Musa akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumwangalia Mungu.


Lakini hautaweza kuniona uso maana hakuna mwanadamu yeyote atakayeniona na kuishi.


Lakini Musa akamwambia Yawe: “Ewe Bwana wangu, mimi mutumishi wako sina ufundi wa kusema tangu zamani, hata kisha kusema nawe. Ulimi wangu ni muzito.”


Lakini Musa akamwambia Yawe: “Angalia, Waisraeli hawanisikilizi mimi. Namna gani mufalme wa Misri atanisikia! Tena mimi ni mutu asiyekuwa na ujuzi wa kuongea!”


Lakini Musa akamwambia Yawe: “Mimi sina ujuzi wa kuongea. Mufalme wa Misri atanisikiliza namna gani?”


Tunasikia nyimbo za sifa kutoka miisho ya dunia, nyimbo za kumusifu Mungu anayekuwa mwenye haki. Lakini mimi ninasema: Ninakonda, kweli ninakonda. Ole kwangu mimi! Wadanganyifu wanaendelea kuwa wadanganyifu, udanganyifu wao unazidi kuwa mubaya zaidi.


Bwana anasema: Watu hawa wanakuja kuniabudu kwa maneno tu, lakini mioyo yao iko mbali nami. Wananiheshimu kulingana na desturi ya watu tu, jambo walilojifunza wao wenyewe.


Mutaweza kumwona mufalme katika utukufu wake, mutaiona inchi anayotawala, kubwa na pana.


Maana mikono yenu imechafuka kwa damu, na vidole vyenu kwa matendo maovu. Midomo yenu imesema uongo, na ndimi zenu zinasema uovu.


Hakuna hata mumoja anayekuja kukuomba; hakuna anayejishugulisha kukutafuta. Wewe unauficha uso wako mbali nasi, umetuacha tufungwe na maovu yetu.


Nami nikajibu: Ee! Bwana wangu Yawe, mimi sijui kusema, ningali bado kijana.


Nitawalewesha wakubwa na wenye hekima wake, watawala wake, maliwali na waaskari wake; watalala usingizi wa milele wala hawataweza tena kuamuka. –Ni ujumbe wa mufalme, jina lake Yawe wa majeshi!


Wewe mwanadamu! Wewe unakaa kati ya watu waasi. Wana macho lakini hawaoni; wana masikio lakini hawasikii.


Basi, wanakuja kwako makundi kwa makundi na kuikaa mbele yako kama watu wangu, kusudi wasikie unachosema, lakini hawafanyi unachowaambia wafanye. Wanasema kwamba wana upendo, lakini hayo ni kusema tu; wanachotafuta kwa moyo ni faida yao tu.


Basi, nilipokuwa nikiomba, nikiitikia zambi zangu na zambi za watu wangu wa inchi ya Israeli, pamoja na kumusihi Yawe kwa ajili ya mulima wake mutakatifu,


Nikasikia hayo, matumbotumbo yangu yakatetemeka. Midomo yangu inatetemeka kwa hofu, mifupa yangu inateguka, miguu yangu inatetemeka. Ninangojea kwa utulivu siku ile ya hasara, ambayo inawafikia wale wanaotushambulia.


Basi, Haruni akafanya kama vile alivyoambiwa na Musa. Akatwaa chetezo chake na kukimbia mpaka katikati ya watu waliokuwa wamekusanyika pamoja. Alipoona kwamba pigo limekwisha kuanza, akatia ubani katika chetezo na kuwafanyia watu upatanisho.


Basi, Manoa akamwambia muke wake: “Hakika tutakufa, maana tumemwona Mungu.”


Halafu Gideoni akatambua kwamba huyo alikuwa malaika wa Yawe; akasema: “Ole wangu, ee Bwana wangu Yawe, maana nimemwona malaika wako uso kwa uso.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ