Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 59:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Hakuna anayemushitaki mwenzake kwa haki, wala anayejitetea kwa ukweli. Munategemea mambo ya bure; munasema uongo. Munafanya mipango ya kuleta hasara na kuzaa uovu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 59:4
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Aache kutumainia udanganyifu, maana udanganyifu ndio utakaokuwa zawadi yake.


Wanatunga udanganyifu na kuzaa uovu. Mioyo yao inapanga udanganyifu.


Kila mumoja anamudanganya mwenzake; anabembeleza lakini ni kwa moyo wa unafiki.


Wanadamu wote ni kama pumzi tu; wote, wakubwa kwa wadogo, hawafai kitu. Wakipimwa wote pamoja, pumzi ni nzito kuliko wao.


Mpaka wakati gani mutanishambulia mimi? Mpaka wakati gani ninyi wote mutanipiga, mimi ninayekuwa kama kiambaza kilichoinama, kama ukuta unaoanza kubomoka?


Mutu mubaya anatunga uovu, anajaa uharibifu na kuzaa udanganyifu.


Waovu hawalali hata kidogo wasipotenda uovu; hawapati usingizi wasipomukwaza mutu.


Ole kwao wanaotunga sheria za uovu, watu wanaopitisha sheria za kugandamiza.


Sisi tulipata maumivu ya kuzaa, lakini tukazaa tu upepo! Hatukupata ushindi wowote kwa ajili ya inchi yetu, hatukuweza kuongeza hesabu ya watu katika inchi.


Ninyi munajidai mumefanya agano na kifo mumefanya mapatano na kuzimu! Ninyi munasema kwamba hasara itakapokuja haitawapata, kwa sababu mumefanya uongo kuwa tegemeo lenu, na udanganyifu kuwa kikingio chenu!


Watesaji watatoweka, wenye kumuchekelea Mungu watakwisha, wote wanaokusudia kutenda maovu watateketezwa.


Kwa hiyo Mungu, Mutakatifu wa Israeli, anasema hivi: Ninyi mumeukataa ujumbe wangu; mukatumainia kutenda mabaya na kutengeneza udanganyifu.


Watu hawa ni waasi, watoto wasioaminiwa; watu wasiopenda kusikia mafundisho ya Yawe.


Mipango yenu yote ni kama maganda, na matokeo yake ni takataka tupu. Pumzi yangu itawaangamiza kama moto.


Hapana! Mawazo yao yameambatana na hicho ambacho ni majivu tu! Mutu huyo amepotoka hata hawezi kujiokoa mwenyewe na kusema: Kweli, hiki ninachokuwa nacho katika mukono wangu ni udanganyifu mutupu!


Ulijiona salama katika uovu wako; ukajisemesha: Hakuna mutu anayeniona. Hekima na elimu yako vilikupotosha, ukajisemesha ndani ya moyo wako: Mimi ndiye; hakuna mwingine isipokuwa mimi.


Ole kwao wanaokokota uovu kama kwa kamba; wanaoburura zambi kama wanavyokokota gari.


Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!


Ukweli umekosekana, naye anayeacha uovu ananyanganywa. Mungu aliona mambo hayo. Alichukizwa kwamba watu hawafuati sheria yake.


Aliona kwamba hakuna mutu aliyejali, akashangaa kwamba hakuna aliyeingilia kati. Basi akaamua kunyoosha mukono wake mwenyewe, haki yake ikamusaidia.


Maana mikono yenu imechafuka kwa damu, na vidole vyenu kwa matendo maovu. Midomo yenu imesema uongo, na ndimi zenu zinasema uovu.


Hata hivyo, ee Yawe, wewe ni Baba yetu. Sisi ni kama udongo, wewe ni mufinyanzi. Sisi wote ni kazi ya mikono yako.


Wale wanaoongoza watu hawa wamewapotosha, na hao wanaoongozwa nao wamepotoka.


Moabu, ulitumainia matendo yako na hazina zako, lakini sasa wewe vilevile utatekwa; mungu wako Kemosi atapelekwa katika uhamisho pamoja na makuhani na watumishi wake.


Mukimbie huko na huko katika Yerusalema, mupeleleze na kujionea wenyewe, muchunguze katika masoko yake. Mukiona hata mutu mumoja anayefuata sheria, mutu anayetafuta ukweli, basi Yawe atausamehe Yerusalema.


Musitumainie maneno haya ya udanganyifu mukisema: Hili ni hekalu la Yawe, hekalu la Yawe, hakika hili ni hekalu la Yawe.


Lakini kumbe, munatumainia maneno ya udanganyifu yasiyokuwa na faida kwenu.


Musikilize maneno ya Yawe, enyi Waisraeli. Yawe anawashitaki wakaaji wa inchi hii. Hakuna tena uaminifu wala wema katika inchi; hakuna anayemujua Mungu katika inchi hii.


Ole wao wanaopanga kutenda maovu, wanaolala usiku wakikusudia mabaya! Mara tu kunapopambazuka, wanayatimiza maana wako na uwezo.


Wayuda wakamwunga mukono, wakisema kwamba maneno yale yote ni ya kweli.


Halafu ile tamaa mbaya ikisha kukomaa, inazaa zambi, nayo zambi ikisha kukomaa inazaa lufu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ