Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 59:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 59:21
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Unijalie kusema ukweli wako siku zote, maana ninatumainia maamuzi yako.


Wewe utaongea naye na kumwambia yote atakayosema. Mimi nitawasaidia na kuwafundisha mambo mutakayofanya.


Uyafunge kwenye vidole vyako; uyaandike ndani ya moyo wako.


Hali itaendelea kuwa hivyo mpaka tujazwe Roho wa Mungu kutoka juu. Hapo jangwa litakuwa shamba lenye udongo muzuri tena, na mashamba yenye udongo muzuri yatakuwa pori.


Majani yananyauka na maua yanafifia, lakini neno la Mungu wetu linadumu milele.


Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.


Yawe anasema hivi: Wakati uliofaa nilijibu maombi yako; wakati wa wokovu nilikusaidia. Nimekuweka na kukufanya ukuwe kiungo cha agano langu na mataifa yote: utatengeneza inchi na kurudisha tena inchi hiyo iliyoharibika.


Nimeyaweka maneno yangu katika kinywa chako; nimekuficha katika kivuli cha mukono wangu. Mimi nilizitandaza mbingu, nikaiweka misingi ya dunia. Mimi ninawaambia, enyi watu wa Sayuni: Ninyi ni watu wangu.


Milima inaweza kutoweka, vilima vinaweza kuondolewa, lakini rehema zangu kwako sitaziacha, agano langu la amani litaimarishwa. Ni Yawe anayekuhurumia anayesema hivyo.


ni vilevile na neno langu mimi: halitanirudilia bila mafanikio, lakini litatimiza mapenzi yangu, litafikia shabaha nililoliwekea.


Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.


Mimi nitawapa amani, amani kwa wanaokuwa mbali na wanaokuwa karibu! –Ni Yawe anayesema hivyo.– Mimi nitawaponyesha.


Kama vile mbingu mupya na dunia mupya nitakazoumba zitakavyodumu milele kwa uwezo wangu, ndivyo wazao wako na jina lako litakavyodumu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Kisha Yawe akanyoosha mukono wake, akagusa kinywa changu, akaniambia: Nimetia maneno yangu ndani ya kinywa chako.


Mimi sikumujua ni nani, lakini yule aliyenituma kubatiza kwa maji aliniambia: ‘Yule utakayemwona Roho akishuka juu yake na kukaa juu yake, mutu yule ndiye anayebatiza kwa Roho Mutakatifu.’


kwa maana nimewatangazia maneno yale uliyoniagiza, nao wameyakubali. Wamejua hakika kwamba nilitoka kwako na kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Aliyetumwa na Mungu anasema maneno ya Mungu, kwa sababu Mungu anamujaza Roho wake kwa uwingi.


lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”


(Alisema vile juu ya Roho atakayepokelewa na wale wanaomwamini Yesu. Kwa wakati ule Roho alikuwa hajatumwa bado, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.)


Mimi ninasema yale niliyoona kwa Baba yangu, lakini ninyi munafanya yale muliyosikia kutoka kwa baba yenu.”


Na hili ndilo agano nitakalofanya nao, wakati nitakapowasamehe zambi zao.”


Lakini ninyi sasa hamutawaliwi na hali yenu zaifu ya kimwili, lakini munatawaliwa na Roho Mutakatifu, ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu. Na mutu yeyote asiyekuwa na Roho wa Kristo ndani yake, yeye si mutu wa Kristo.


Basi si zaidi sana matokeo ya utumishi wa Roho yatakuwa yenye utukufu?


“Hili ndilo agano nitakalofanya nao nyuma ya siku zile. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo. Nitawawezesha kuchunga sheria zangu ndani ya mafikiri, nikiziandika ndani ya mioyo yao.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ