Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 59:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Atawaazibu waadui kadiri ya matendo yao, kasirani yake na kisasi vitawapata waadui zake; atawaazibu hata wakaaji wa inchi za mbali.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 59:18
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu atamulipa mutu kadiri ya matendo yake, atamulipiza kulingana na mwenendo wake.


Mungu amesema mara na mara, nami nimesikia tena na tena kwamba uwezo ni wa Mungu.


Kwa hiyo, nitawamwangia waadui zangu hasira yangu, nitawalipiza kisasi wapinzani wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–


Muwaambie waliovunjika moyo: Mujipe moyo, musiogope! Muangalie Mungu wenu atakuja kulipiza kisasi, atakuja kuwaazibu waadui zenu; atakuja yeye mwenyewe kuwaokoa ninyi.


Bwana wetu Yawe anakuja na nguvu, kwa mukono wake anatawala. Yeye anakuja na mapato yake, anafika na mushahara wake.


Lakini mimi nikafikiri: Nimeshugulika bure, nimetumia nguvu zangu bure kabisa. Hata hivyo, Yawe atanipa haki yangu; mushahara wa kazi yangu uko kwa Mungu.


Kweli, nimekamua mizabibu peke yangu, wala hakuna mutu aliyekuja kunisaidia. Nimeyakanyaga mataifa kwa hasira yangu, niliyapondaponda kwa kasirani yangu. Nguo zangu zimejaa madoa ya damu yao, imechafua kabisa nguo yangu.


Kwa hasira yangu niliwaponda watu, niliwalewesha kwa kasirani yangu; damu yao niliimwanga chini.


Mujue kwamba mambo hayo yameandikwa mbele yangu, sitanyamaza lakini nitawalipiza; nitawalipa sawa inavyostahili.


Nitawalipiza maovu yao wayalipe vilevile maovu ya babu zao. –Ni Yawe anayesema hivyo.– Wao waliifukizia ubani miungu yao kwenye milima, wakanitukana mimi kule juu ya vilima. Nitawalipa sawa inavyostahili, watayalipa matendo yao ya zamani.


Mutayaona hayo na mioyo yenu itafurahi; mifupa yenu itastawi tena kama vile majani mabichi. Kwa hiyo itajulikana kwamba mimi Yawe ninawalinda watumishi wangu, lakini nikikasirika ninawaazibu waadui zangu.


Yawe atakuja kama moto, na magari yake ya vita ni kama zoruba. Ataiacha hasira yake ifanye kazi yake kwa ukali, na maonyo yake yatimizwe kwa ndimi za moto.


Musikilize: makelele kutoka katika muji, sauti kutoka katika hekalu! Hiyo ni sauti ya Yawe akiwaazibu waadui zake!


Mimi Yawe ninapima akili na kuchunguza moyo wa mutu. Na hivyo ninamutendea kila mumoja, kulingana na mwenendo wake, kadiri ya matendo yake.


Wewe unapanga kwa hekima na unafanya maajabu; njia za watu wote ziko wazi mbele yako, unamulipa kila mumoja kadiri ya njia zake na matendo yake.


Mupigie kelele za vita pande zote; sasa Babeli umejitoa ukamatwe. Vikingio vyote vimeanguka, kuta zake zimebomolewa. Ni malipizi ya Yawe. Basi muulipize kisasi. Muutendee kama vile ulivyotendea wengine.


Muwaite wapiga mishale waishambulie Babeli. Mupeleke kila mutu anayejua kuvuta upinde. Muuzunguke muji kusikuwe mutu yeyote atakayetoroka. Muulipize kadiri ya matendo yake yote; muutendee kama ulivyowatendea wengine, maana kwa kiburi ulinizarau mimi Yawe, Mutakatifu wa Israeli.


Yawe ameonyesha kabisa kasirani yake, aliimwanga hasira yake kali, aliwasha moto huko katika Sayuni ambao uliteketeza misingi yake.


Na ninyi Ohola na Oholiba, mutaazibiwa kutokana na uzinzi wenu na zambi yenu ya kuziabudu sanamu za miungu. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Bwana wenu Yawe.


Siku ile Gogi atakapoishambulia inchi ya Israeli, nitawakisha kasirani yangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Ndivyo nitakavyomaliza hasira yangu, nami nitakuwa nimetuliza kasirani yangu na kufarijika ndani ya moyo. Hapo ndipo watakapojua kwamba mimi, Yawe, nimewaazibu kwa sababu ya wivu wangu kwa ukosefu wenu wa uaminifu.


Anayekuwa mbali sana atakufa kwa ugonjwa mukali. Anayekuwa karibu atauawa kwa upanga. Atakayekuwa amebaki na kuponyoka hayo mawili atakufa kwa njaa. Ndivyo nitakavyotimiza kasirani yangu juu yao.


Jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa kama damu, mbele ya kutimia kwa siku ya Yawe, siku inayokuwa kubwa na ya kutisha.


basi nami nitapingana nanyi kwa hasira kali, na kuwaazibu mimi mwenyewe mara saba zaidi kwa ajili ya zambi zenu.


Yawe ni Mungu mwenye wivu, anayelipiza kisasi; Yawe analipiza kisasi na ni mwenye kasirani; Yawe analipiza kisasi kwa wapinzani wake, kasirani yake inawaka juu ya waadui zake.


Kwa maana Mwana wa Mutu atakuja na wamalaika akitukuzwa na Baba yake, halafu atamulipa kila mutu kufuatana na matendo yake.


Na sasa kwa ngambo ya wale waadui zangu walionikataa mimi kuwa mufalme wao, muwalete hapa na kuwaua mbele yangu.’ ”


Kwa maana siku zile zitakuwa siku za azabu ya Mungu, kusudi mambo yote yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu yatimie.


Kwa maana Mungu atamulipa kila mutu kwa kadiri ya matendo yake.


nitanoa upanga wangu unaometemeta, nitanyoosha mukono kutoa hukumu, nitawalipiza kisasi waadui zangu, nitawaazibu wale wanaonichukia.


Na ule muji mukubwa ukagawanyika katika sehemu tatu, na miji ya mataifa yote ikabomoka. Mungu hakusahau muji mukubwa Babeli, akaukunywesha kikombe kinachokuwa na divai ya kasirani yake kali.


Ndani ya kinywa chake mulitoka upanga mukali kwa kushinda mataifa. Naye atatawala kwa fimbo ya chuma na kukamua zabibu ndani ya kikamulio cha divai kinachojaa kasirani kali ya Mungu Mwenye Uwezo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ