Isaya 59:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
16 Aliona kwamba hakuna mutu aliyejali, akashangaa kwamba hakuna aliyeingilia kati. Basi akaamua kunyoosha mukono wake mwenyewe, haki yake ikamusaidia.
Nilipokuja, kwa nini sikukuta mutu? Nilipoita mbona hamukuitikia? Mukono wangu ni mufupi hata nisiweze kuwaokoa ninyi? Sina nguvu ya kuwakomboa? Ninakausha bahari kwa kuikaripia, na mito ninaifanya kuwa jangwa; samaki wake wanakufa na kunuka kwa kukosa maji.
Amuka! Amuka na nguvu, ee mukono wa Yawe! Amuka kama ulivyofanya hapo zamani, nyakati za vizazi vilivyopita. Si wewe ndiwe uliyemukatakata yule nyama mukubwa Rahabu, ukamutoboa yule nyoka mukubwa wa kuogopesha?
Yawe ameapa kwa uwezo wake mukubwa, ameapa kwa nguvu yake akisema: Sitawapa tena waadui zako ngano yako; wala wageni hawatakunywa tena divai yako ambayo umeitoshea jasho.
Mukimbie huko na huko katika Yerusalema, mupeleleze na kujionea wenyewe, muchunguze katika masoko yake. Mukiona hata mutu mumoja anayefuata sheria, mutu anayetafuta ukweli, basi Yawe atausamehe Yerusalema.
Nilitafuta kati yao mutu mumoja atengeneze ukuta na kusimama juu ya nafasi iliyobomoka mbele yangu, kusudi ailinde inchi na kunizuia nisiiharibu, lakini sikumupata hata mumoja.