Isaya 59:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
13 Tumekuasi na kukukana, ee Yawe, tumekataa kukufuata, ewe Mungu wetu. Tunasema maneno ya kutesa na uasi, katika mioyo yetu tunatunga na kutoa maneno ya uongo.
Wapumbafu wanasema maneno ya upumbafu, na mafikiri yao ni kutenda maovu, kutenda mambo ya watu wasiomujua Mungu, kusema maneno ya kumutukana Yawe. Wanawaacha wenye njaa bila chakula, na wenye kiu wanawanyima kinywaji.
Haujapata kuyasikia wala kuyajua hata kidogo; tangu zamani masikio yako hayakuyasikia. Nilijua kwamba wewe ni mudanganyifu, na kwamba wewe ni mwasi tangu kuzaliwa.
Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!
Mulimwogopa na kutishwa na nani hata mukasema uongo, mukaacha kunikumbuka mimi na kuacha kabisa kufikiri juu yangu? Mimi sikuwaambia kitu kwa muda murefu; ndiyo maana labda mukaacha kuniheshimu!
Kama ukiacha kufanya kazi siku ya Sabato, ukiacha shuguli zako siku yangu hiyo takatifu, ukiifanya siku yangu kuwa ya furaha, ukiheshimu siku hiyo takatifu ya Yawe, ukiacha shuguli zako au kupiga domo,
Kila siku wananitafuta, wanatamani kujua njia zangu, kama vile wao ni taifa linalotenda haki, taifa lisilosahau agizo la Mungu wao. Wanataka niamue kwa haki, na kutamani kuikaa karibu na Mungu.
Halafu mutaomba, nami Yawe nitawaitikia; mutalia kwa sauti kwa kuomba musaada, nami nitajibu hivi: Niko hapa! Kama mukiondoa mambo ya kitumwa, mukiacha kuzarau wengine na kusema maovu,
Ee Yawe, tumaini la Waisraeli, wote wanaokukataa wafezeheshwe. Wanaokuacha wewe watatoweka, kama majina yaliyoandikwa chini katika mavumbi, kwa maana wamekuacha wewe Yawe, unayekuwa chemichemi ya maji ya uzima.
mumepotoka, mumeyahatarisha maisha yenu. Maana mulinituma kwa Yawe, Mungu wenu, mukiniambia: Utuombee kwa Yawe, Mungu wetu kwamba kitu chochote Yawe, Mungu wetu, atakachosema, utuambie, nasi tutatimiza.
Halafu wale walioponyoka watanikumbuka katikati ya mataifa ambamo watakuwa wamepelekwa katika uhamisho. Nitakuwa nimewavunja moyo wao wa uzinzi ambao ulinitupilia mbali, na macho yao yaliyozini na sanamu zao. Kwa hiyo watajichukia wao wenyewe kwa sababu ya maovu na machukizo yao yote waliyoyatenda.
Yawe alipoanza kusema na Waisraeli kwa njia ya Hosea, alimwambia hivi: Kwenda kuoa mwanamuke muzinzi, uzae naye watoto wa uzinzi, maana watu wa inchi hii wanafanya uzinzi mwingi kwa kuniacha mimi.
Kila mara nikitaka kurudishia watu wangu hali yao ya mbele, ninapotaka kuwaponyesha Waisraeli, uovu wa watu wa Efuraimu unafunuliwa, matendo mabaya ya Samaria yanajitokeza. Wao wanaongozwa na udanganyifu, mwizi anabomoa nyumba; inje katika barabara wanyanganyi wanashambulia.
Farasi wanaweza kukimbia katika mawe makubwa? Watu wanaweza kulima bahari na ngombe? Lakini ninyi mumeigeuza sheria kuwa sumu, na tunda la haki kuwa uchungu.
Basi wandugu zangu, muangalie vizuri, kati yenu kusikuwe mutu mumoja mwenye moyo mubaya wa kutokuamini, aliyefikia hata kujitenga mbali na Mungu Mwenye Uzima.
Nao ulimi ni kama moto. Ulimi ni kiungo kinachojaa ubaya wa kila namna. Ulimi unapatikana kwenye nafasi yake katikati ya viungo vyetu, nao ndio unaochafua mwili wote. Unateketeza maisha yetu ukichomwa wenyewe na moto unaotoka katika jehenamu.
Halafu akawaambia watu wote: “Jiwe hili ndilo litakalokuwa ushuhuda kwetu, maana limesikia maneno yote ambayo Yawe ametuambia. Kwa hiyo, litashuhudia juu yenu, kusudi musipate kumwasi Mungu wenu.”