Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 59:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Tunanguruma kama dubu, tunaomboleza kama njiwa. Tunatazamia watu wanaofuata sheria ya Mungu, lakini hakuna, tunatazamia wokovu, lakini uko mbali nasi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 59:11
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wale wanaonitesa vibaya wanakaribia, hao wako mbali kabisa na sheria yako.


Waovu hawataokolewa hata kidogo, maana hawajali juu ya masharti yako.


Viungo vyangu vimeshambuliwa na homa; hakuna uzima katika mwili wangu.


Ee Mungu, tega sikio usikie maombi yangu; usiangalie pembeni ninapokuomba.


Ninasikiliza yale Yawe anayosema, maana anaahidi kuwapa watu wake amani, watu wake mwenyewe wasiporudilia upumbafu wao.


Ninalia kama mbaruwayi, ninaugua kama njiwa. Macho yangu yamefifia kwa kuangalia juu. Ee Bwana, ninateseka; ukuwe wewe usalama wangu!


Watoto wako wamezimia, wamelala pembeni ya kila barabara, wako kama paa aliyenaswa ndani ya mutego. Wamepatwa na kasirani ya Yawe, wamepatwa na azabu ya Mungu wako.


Sheria ya Mungu imewekwa pembeni, haki iko mbali; ukweli unakanyagwa katika tribinali, usawa hauwezi kuingia humo.


Njia ya amani hamuijui hata kidogo; hamufuati sheria ya Mungu. Mumejifanyia njia potovu, yeyote anayepitia humo hapati amani.


Kwa hiyo, kufuata sheria ya Mungu kuko mbali nasi, haki haifiki kwetu. Tulitazamia kupata mwangaza, kumbe ni giza tupu; tulingojea mwangaza, lakini tunatembea katika giza.


Tulitazamia kupata amani lakini hakuna kitu kizuri. Tulitazamia kupona lakini tumepatwa na vitisho.


Heri ningepata kibanda cha wasafiri katika jangwa, ningewaacha watu wangu na kujiendea. Wote ni wazinzi, ni kundi la watu waasi.


Moyo wangu haujui tena amani, nimesahau furaha.


Ikiwa kuna watu walioponyoka, watakimbilia kwenye milima kama njiwa waliotishwa katika bonde. Kila mumoja wao ataomboleza kwa ajili ya zambi zake.


Wananililia, lakini si kwa moyo. Wanagaagaa na kujikatakata juu ya vitanda vyao, kusudi nisikilize maombi yao kwa kupata ngano na divai; lakini wanaendelea kuniasi.


Vikingio vya mito vimefunguliwa, nyumba ya kifalme imejaa hofu.


Muji uko wazi kabisa, watu wamekamatwa mateka. Wanawake wake wanaomboleza, wanalia kama njiwa, na kujipigapiga kwenye vifua.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ