Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 58:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mafungo ya kweli ni kugawanya chakula chako pamoja na wenye njaa, kuwakaribisha katika nyumba yako wamasikini wasiokuwa na makao, kuwavalisha wasiokuwa na nguo, bila kusahau kuwasaidia wandugu zenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 58:7
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Loti akawaendea wachumba wa wabinti zake, akawaambia: “Haraka! Mutoke pahali hapa, maana Yawe atauangamiza muji huu.” Lakini wao wakamwona kama mutu mwenye kuchekesha tu.


Akasema: “Bwana zangu, karibu katika nyumba yangu mimi mutumishi wenu. Munaweza kunawa miguu na kulala kwangu usiku wa leo. Asubui mapema mutaweza kuendelea na safari yenu.” Lakini, wao wakasema: “Hapana! Sisi tutalala huku katika barabara.”


Wale wakubwa waliotajwa majina yao waliwatwaa wafungwa na kwa kutumia vitu vilivyonyanganywa wakawavalisha wafungwa ambao hawakukuwa na nguo; waliwapatia viatu, chakula na vinywaji, na kuwapakaa mafuta. Wale ambao walikuwa hawajiwezi, wakawabeba juu ya punda, wakawapeleka wafungwa wote mpaka Yeriko, muji wa mingazi, kwa wandugu zao; kisha wao wakarudi Samaria.


Lakini sisi ni sawa na Wayuda wengine; watoto wetu ni sawa na watoto wao. Hata hivyo, tunawalazimisha watoto wetu kuwa watumwa. Wabinti zetu wamoja wamekwisha kuwa watumwa. Hatuna uwezo wa kuzuia jambo hili maana mashamba yetu na mizabibu yetu inanyanganywa na watu wengine.”


Umewanyima maji wale waliokuwa wamechoka; umewanyima chakula wale wanaokuwa na njaa.


Anatoa kwa moyo safi, anawapa wamasikini. Haki yake inadumu milele. Ana nguvu na sifa.


Mutu mwema anafaidika yeye mwenyewe, lakini mutu mukali anajiumiza mwenyewe.


Mutu mwenye kuwa tayari kusaidia atabarikiwa, maana anagawanya chakula chake na masikini.


Umwokoe mutu anayepelekwa kuuawa kwa bure; usisite kumwopoa anayeuawa bila kosa.


Adui yako akiwa na njaa, umupe chakula; akiwa na kiu, umupe maji ya kunywa.


Anayesaidia wamasikini hatakosewa kitu, lakini anayekataa kuwaangalia atalaaniwa kwa wingi.


mukiwapa wenye njaa chakula, mukitimiza mahitaji ya wenye kuteswa, mwangaza utawaangazia nyakati za giza, giza lenu litakuwa kama muchana.


Yawe anasema hivi: Mufuate sheria yangu na kutenda kwa haki. Muokoe kila mutu aliyenyanganywa mali zake toka katika mikono ya mutesaji. Musiwatendee vibaya au kwa ukali wageni, wayatima na wajane, wala musimwange damu ya mutu asiyekuwa na kosa kwa nafasi hii.


Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!


Basi muwasaidie wamasikini na vitu vya ndani, na vingine vyote vitakuwa safi kwenu.


Lakini Zakayo akasimama mbele ya Bwana na kumwambia: “Bwana! Ninawapa masikini nusu ya mali zangu, na kama nimetwaa kitu cha mutu kwa kumudanganya, nitamurudishia mara ine sawa na kitu kile.”


Naye akawajibu: “Mwenye kuwa na kanzu mbili atoe moja kwa yule asiyekuwa na kitu, na anayekuwa na vyakula afanye hivi vilevile.”


Kisha yeye na watu wa nyumba yake wakabatizwa. Naye akatusihi akisema: “Ikiwa munakubali kweli kwamba ninamwamini Bwana, basi mufike mupange ndani ya nyumba yangu.” Akatulazimisha tuitike.


Kisha akapeleka Paulo na Sila ndani ya nyumba yake na kuwapatia chakula. Yeye pamoja na watu wote wa nyumba yake walifurahi sana kwa sababu wamemwamini Mungu.


Muwasaidie watu wa Mungu katika mahitaji yao na muwakaribishe wageni.


“Ukimwona ngombe au kondoo wa ndugu yako amepotea, usimwache, lakini umurudishe kwa ndugu yako.


Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.


Ndugu, upendo wako umenifurahisha sana na kunifariji, kwa maana umetuliza mioyo ya watu wa Mungu.


“Museme hapa hapa mbele ya wanainchi wote wa Sekemu: Jambo gani ni jema kwenu, kwamba watoto wote makumi saba wa kiume wa Yerubali wawatawale au mutoto mumoja? Mukumbuke kwamba mimi ni damu yenu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ