Isaya 58:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Yawe anasema: Piga kelele, wala usijizuize; ulalamike kwa sauti kubwa kama baragumu. Uwatangazie watu wangu makosa yao, uwaambie wazao wa Yakobo zambi zao.
Siku hiyo, baragumu kubwa itapigwa na watu wote wa Israeli waliopotea katika inchi ya Asuria au waliotawanywa katika inchi ya Misri watarudi na kumwabudu Yawe juu ya mulima mutakatifu kule Yerusalema.
Yawe anasema hivi: Kama nimeachana na mama yako Yerusalema, barua ya kuachana iko wapi? Nilikuwa na deni ya nani kwa kuwauzisha? Mukumbuke kwamba muliuzishwa kwa ajili ya maovu yenu, mama yenu alifukuzwa kwa ajili ya makosa yenu.
Maana walinzi wa Israeli wote ni vipofu; wote hawana akili yoyote. Wote ni kama imbwa bubu wasioweza kufoka, wanalala tu na kuota ndoto, wanapenda sana kusinzia!
Kwenda uwatangazie waziwazi wakaaji wote wa Yerusalema na kusema hivi: Yawe anasema hivi: Ninakumbuka wema wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama muchumba wako. Ulinifuata katika jangwa kwenye inchi ambayo haikupandwa kitu.
Katika mwaka wa tano wa utawala wa mufalme Yoyakimu wa Yuda mwana wa Yosia, katika mwezi wa kenda, wakaaji wote wa Yerusalema na watu wote waliofika Yerusalema kutoka miji ya Yuda, walitangaza siku ya kufunga kula chakula mbele ya Yawe.
Manabii wako wamekuonea maono madanganyifu. Hawakufichua wazi uovu wako kusudi wapate kukurudishia hali yako ya mbele. Lakini walikuonea maono ya uongo na ya kupotosha.
Nyuma ya mambo hayo nilipata maono mengine. Niliona mulango mumoja umefunguliwa wazi mbinguni. Halafu ile sauti niliyosikia mara ya kwanza, iliyolia kama baragumu, ikaniambia: “Panda huku, nami nitakuonyesha mambo yanayopaswa kutokea nyuma ya hayo ya mbele.”