Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 57:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Ni nani munayemuchekelea? Munamuzomea nani na kumutoshea ulimi inje? Ninyi wenyewe ni waasi tangu mwanzo, ninyi ni kizazi kidanganyifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 57:4
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.


Waadui wengi wananizunguka kama ngombe dume; wamenisonga kama ngombe dume wanono wa Basani!


Kundi la waovu limenizunguka; wananizunguka kama kundi la imbwa; wamenitoboa mikono na miguu.


Lakini mimi ni mududu tu, wala si mutu; nimetukaniwa na kuzarauliwa na watu.


Wananishitaki kwa sauti, wakisema: “Sawa! Sawa! Tumeona wenyewe uliyotenda!”


Nilipovaa gunia kwa kuomboleza, nikageuka kuwa wimbo kwao.


Lakini ungali unaonyesha kiburi juu ya watu wangu, wala hauwaachi waondoke.


Ole kwako wewe taifa lenye zambi, watu waliolemewa na uovu, kizazi cha watenda mabaya, watoto wanaoishi kwa udanganyifu! Ninyi mumemwacha Yawe, mumemuzarau Mutakatifu wa Israeli, mumerudi nyuma.


Shoka litaweza kujisifu mbele ya yule anayelitumia? Musumeno unaweza kujivuna mbele ya mwenye kukata nao? Ni kama kwamba vile fimbo ingeweza kumwinua anayeishika, au gongo kumwinua mwenye kuitumia!


Ole watoto waasi, wanaotimiza mipango yao na si mipango yangu, wanaofanya mapatano kinyume cha mapenzi yangu! –Ni ujumbe wa Yawe.– Kweli, wanalundika zambi juu ya zambi.


Watu hawa ni waasi, watoto wasioaminiwa; watu wasiopenda kusikia mafundisho ya Yawe.


Wewe umemutukana nani? Umemutusi nani? Umesubutu kumufokea nani kwa majivuno? Ni Mungu, Mutakatifu wa Israeli!


Kwa vile umefanya mipango juu yangu na nimesikia majivuno yako, nitatia ndoana yangu ndani ya pua yako, na lijamu yangu ndani ya kinywa chako. Nitakurudisha katika njia ileile uliyokuja ndani yake.


Haujapata kuyasikia wala kuyajua hata kidogo; tangu zamani masikio yako hayakuyasikia. Nilijua kwamba wewe ni mudanganyifu, na kwamba wewe ni mwasi tangu kuzaliwa.


Ninyi munawaka tamaa kwenye miti ya mialo, na chini ya kila muti wenye kuwa na majani mabichi. Munawachinja watoto wenu na kuwatambikia katika mabonde na ndani ya nyufa za mawe.


Kila mara ninaposema kitu, ninalalamika, ninapandisha sauti kwa kutangaza mateso na uharibifu. Kutangaza neno la Yawe kunaniletea kuzomewa na kuzarauliwa kila siku.


Watu hao ni wenye kichwa nguvu na moyo mugumu. Ninakutuma kwao, nawe utawaambia: “Bwana wetu Yawe anasema hivi.”


Enyi Waisraeli, ninyi mumetenda zambi tangia kule Gibea, na mpaka sasa munaendelea. Hakika vita itawaangamizia kulekule Gibea.


Si Haruni tu munayemunungunikia, wewe na kundi lako, lakini kwa kweli munamwasi Yawe.


Shamba ni dunia. Mbegu nzuri ni washiriki wa Ufalme. Nyasi ni washiriki wa yule Mwovu Shetani.


Nao wakasokota taji na tawi lenye miiba na kumuvalisha nalo kwenye kichwa chake. Wakaweka tete katika mukono wake wa kuume, wakapiga magoti mbele yake na kumuchekelea, wakisema: “Jambo, Mufalme wa Wayuda!”


Yesu akaongeza kuwaambia wanafunzi wake: “Yule anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; yule asiyewapokea ninyi, hanipokei mimi, na yule asiyenipokea mimi, hamupokei yule aliyenituma.”


Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo, sababu gani unanitesa?”


Mutu asiwadanganye na maneno yasiyokuwa na maana; kwa sababu ya makosa kama hayo, Mungu anawaazibu kwa kasirani yake wale wasiomutii.


Kwa sababu ya makosa haya, kasirani ya Mungu itawaangukia wale wanaomwasi.


Nyuma ya hayo Waisraeli wote wakarudi salama kwa Yoshua kule katika kambi Makeda; na hakuna tena mutu aliyesubutu kusema neno lolote juu ya Waisraeli.


Watalipwa mateso kwa sababu ya mateso waliyoleta. Wanafurahia kutimiza waziwazi tamaa zao mbaya za kimwili muchana kati. Kufika kwao katika karamu zenu kunaleta haya na chukizo kubwa wanapofurahia mambo yao ya udanganyifu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ