Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 57:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 kusudi apate kuingia kwenye amani. Watu wenye mwenendo sawa, watakuwa na amani na kupumzika.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 57:2
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.


Akazikwa katika kaburi alilokuwa amejichimbia yeye mwenyewe, katika muji wa Daudi. Walimulalisha juu ya kitanda kilichokuwa kimejazwa marasi ya kila aina yaliyotayarishwa na wafundi wa kutengeneza marasi, wakawasha moto mukubwa sana kwa heshima yake.


Kule kwa wafu waovu hawasumbui mutu, kule wanaochoka wanapumzika.


Muangalie mutu mukamilifu, mutu wa usawa; mutu anayependa amani anajaliwa wazao.


mavumbi yanarudilia inchi tena, na roho inamurudilia Mungu aliyeipana.


Wafalme wote wa mataifa wamezikwa kwa heshima kila mumoja ndani ya kaburi lake.


Njia ya watu wa haki ni yenye kunyooka; ewe Mungu mwenye haki, unasawanisha njia yao.


Yawe anasema hivi: Musimame katika masanganjia, muangalie. Muulize juu ya matukio ya zamani. Mutafute pahali panapokuwa njia nzuri muifuate, nanyi mutaweza kupumzika. Lakini wao wakasema: Hatutafuata njia hiyo.


Elamu imelalishwa kati ya wale waliouawa katika vita. Makaburi yao yanaizunguka. Wote waliuawa katika vita, bila kujua Mungu. Walipokuwa wangali wanaishi, walieneza vitisho vyao katika inchi ya wanaokuwa wazima, na sasa wako wanapata haya yao pamoja na wale wanaoshuka katika shimo kwa wafu. Wanawekwa kati ya wale waliouawa.


Lakini wewe, ee Danieli, ujiendee, upumzike katika kaburi, na wakati huo utakapotimia, utafufuka na kupata zawadi yako.


Bwana wake akamwambia: ‘Ni vizuri, wewe mutumishi mwema na mwaminifu. Ulikuwa mwaminifu katika ulinzi wa mali ndogo, basi nitakuweka kuwa mulinzi wa mali mengi. Kuja ufurahi pamoja na bwana wako.’


Wote wawili walikuwa wenye haki mbele ya Mungu, walishika kwa ukamilifu amri na maagizo yote ya Bwana.


Siku moja yule masikini akakufa, na wamalaika wakamupeleka mpaka pembeni ya Abrahamu. Na yule tajiri akakufa vilevile na kuzikwa.


“Sasa, Ee Bwana, umuruhusu mutumishi wako akufe katika amani, maana umetimiza ahadi yako.


Lakini Yesu akamwambia tena yule mwanamuke: “Kwenda na amani, imani yako imekuokoa.”


Kwa maana, tunajua kwamba hema hii tunayoishi ndani yake hapa katika dunia, maana yake mwili wetu, itakapobomolewa, Mungu atatupatia makao mengine mbinguni. Nayo ni nyumba aliyoijenga yeye mwenyewe na inayodumu milele.


Sisi tuna uhodari na tungependa zaidi kutoka katika mwili huu na kwenda kuishi pamoja na Bwana.


Maana ninasongwa na mambo mawili. Ninatamani kujiendea na kukaa pamoja na Kristo, maana hili ndilo jambo bora zaidi.


Tena nikasikia sauti kutoka mbinguni, ikisema: “Andika maneno haya: ‘Heri tangu sasa kwa watu wanaokufa wakimwamini Bwana!’ ” Naye Roho anasema: “Ndiyo, ni kweli. Watapumzika toka katika masumbuko yao, kwa maana matendo yao yatafuatana nao.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ