Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 57:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Mimi nitawapa amani, amani kwa wanaokuwa mbali na wanaokuwa karibu! –Ni Yawe anayesema hivyo.– Mimi nitawaponyesha.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 57:19
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe, ee Yawe, umetupatia amani; umefanikisha shuguli zetu zote.


Ee Mungu, unawaweka katika amani wanaokuwa imara, unawaweka katika amani kwa sababu wanakutegemea.


Kutokana na kutenda kwa haki, watu watapata amani, utulivu na usalama kwa milele.


Bwana wetu Yawe amenifundisha jinsi ya kusema, kusudi niwatie moyo wale waliochoka. Kila asubui ananipa hamu ya kusikiliza mambo anayotaka kunifundisha.


Nimeyaweka maneno yangu katika kinywa chako; nimekuficha katika kivuli cha mukono wangu. Mimi nilizitandaza mbingu, nikaiweka misingi ya dunia. Mimi ninawaambia, enyi watu wa Sayuni: Ninyi ni watu wangu.


Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.


Naye akinigusa nalo kwenye mudomo, akasema: Kaa hili limekugusa kwenye mudomo; umeondolewa kosa lako, umesamehewa zambi yako.


Sasa wanakuita wewe Sayuni: “Aliyetupiliwa”, “Muji usioshugulikiwa na mutu”. Lakini nitakurudishia afya yako, nitaponyesha vidonda vyako. –Ni ujumbe wa Yawe.


Hata hivyo, mimi nitauponyesha muji huu na kuwapa watu wake afya; nitawajalia ustawi mwingi na usalama.


Enyi Waisraeli, mumurudilie Yawe, Mungu wenu. Mumejikwaa kwa sababu ya uovu wenu.


Yawe anasema: Nitaponyesha ukosefu wao wa uaminifu; nitawapenda tena kwa moyo wangu wote, maana sitawakasirikia tena.


Wakati huo nitabadilisha luga ya watu, nitawawezesha kusema luga safi kusudi waniite mimi Yawe, na kuniabudu kwa moyo mumoja.


Ataondoa kabisa magari ya vita katika inchi ya Efuraimu, na farasi wa vita kutoka katika Yerusalema; pinde za vita zitatupwa mbali. Naye ataleta amani kati ya mataifa; utawala wake utaenea toka bahari mpaka bahari, toka muto Furati hata miisho ya dunia.


Kama watu wa nyumba ile wakiwakaribisha, wakuwe na amani ile muliyowatakia, lakini wasipowakaribisha, amani ile iwarudilie.


Kisha akawaambia: “Mwende katika dunia yote na kuhubiri Habari Njema kwa kila mutu.


“Sifa kwa Mungu juu mbinguni, na amani katika dunia kwa watu anaowapenda.”


Kwa maana mimi mwenyewe nitawapa masemi na hekima hata waadui zenu hawataweza kuyapinga wala kuyakataa.


Yeye ametuma ujumbe wake kwa Waisraeli, akiwahubiri Habari Njema ya amani kwa njia ya Yesu Kristo, anayekuwa Bwana wa watu wote.


Kwa maana ahadi hii ya Mungu ilitolewa kwenu, kwa watoto wenu na kwa wote wanaokaa mbali, ndio wote ambao Bwana Mungu wetu atakaowaita.”


Lakini sasa, katika kuungana kwenu na Yesu Kristo, ninyi muliokuwa mbali, mumekuwa karibu kwa njia ya damu ya Kristo.


Muniombee vilevile, kusudi Mungu anijalie maneno ya kusema. Kwa hiyo nitaweza kuwajulisha watu kwa uhodari siri ya Habari Njema.


Basi kwa njia ya Yesu, tumutolee Mungu sadaka za kumusifu siku zote, maana yake kutangaza kwamba tunaaminia jina lake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ