Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 57:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Yawe anasema hivi: Mujenge! Mujenge! Mutayarishe njia! Muondoe vikwazo vyote katika njia ya watu wangu!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 57:14
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini watu wa haki wanafurahi Mungu anapokuja, wanashangilia na kuimba kwa furaha.


Humo kutakuwa barabara kubwa, nayo itaitwa Njia Takatifu. Watu wachafu hawatapitia humo, lakini wale watu wa Mungu tu; wapumbafu hawatakanyaga ndani yake,


Sauti inatangaza katika jangwa: Mutengenezee Yawe njia, munyooshe barabara kubwa kwa ajili ya Mungu wetu.


Milima yote nitaifanya kuwa njia, na barabara zangu kubwa nitazitengeneza.


Enyi wakaaji wa Yerusalema, mutoke, mutoke inje ya muji, muwatayarishie njia watu wenu wanaorudia! Mujenge! Mujenge barabara na kuondoa mawe yote! Muweke bendera kuwa kitambulisho kwa ajili ya watu.


Lakini watu wangu wamenisahau mimi, wanaifukizia miungu ya uongo ubani. Wamejikwaa katika njia zao, wameacha barabara zao za zamani.


Basi tusihukumiane tena sisi wenyewe. Lakini tafazali mukamate kusudi hili: mutu asifanye kitu kinachoweza kumukwaza au kumwangusha ndugu yake katika zambi.


Lakini sisi tunamuhubiri Kristo aliyetundikwa juu ya musalaba, na mahubiri hayo yanahesabiwa kama kikwazo kwa Wayuda na upumbafu kwa watu wa mataifa mengine.


Kwa hiyo chakula kikimwangusha ndugu yangu katika zambi, nitajizuiza kula nyama siku zote kusudi nisimwangushe ndugu yangu.


Lakini, muangalie vizuri kusudi uhuru wenu usiangushe wale wanaokuwa zaifu katika imani.


Sisi hatutaki kumukwaza mutu yeyote katika jambo lolote kusudi kazi yetu isizarauliwe.


Mujitengenezee njia zenye kunyooka, kusudi mwenye ulema wa miguu asiteguke, lakini apate kupona.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ