Wewe umejichokesha bure na washauri wako. Basi, wajitokeze hao wenye akili wakuokoe! Wao wanagawanya mbingu sehemusehemu, wanachunguza nyota na kutabiri kila mwezi yatakayokupata.
Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.