Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 56:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mugeni anayenitambua mimi Yawe asifikiri hivi: Hakika Yawe atanitenga na watu wake. Naye towashi asiseme: Mimi ni muti wenye kukauka!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 56:3
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Na hata mugeni asiyekuwa Mwisraeli atakayekuja kutoka inchi ya mbali kwa ajili ya jina lako kubwa, na juu ya nguvu na ulinzi wako, akikuja kuomba katika nyumba hii,


Wayuda wakaifanya kuwa sheria kwao, kwa wazao wao na kwa mutu yeyote ambaye angejiunga nao, kwamba katika wakati uliopangwa kila mwaka, bila kukosa, siku hizo mbili zishikwe kulingana na maagizo ya Mordekayi.


Yawe atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawachagua tena Waisraeli. Atawarudisha katika inchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.


Tena wamoja kati ya watoto wako wanaume watapelekwa, nao watakuwa matowashi watakaotumika katika nyumba ya mufalme wa Babeli.


nitamupatia nafasi ya ukumbusho na ya sifa katika nyumba yangu na kuta zangu, nafasi bora kuliko kuwa na wana na wabinti. Nitamupatia jina la kukumbukwa siku zote na ambalo halitafutwa hata kidogo.


Wageni watakaoshikamana nami Yawe, kwa kunitumikia na kwa kupenda jina langu, na kuwa watumishi wangu, wote watakaoshika siku ya Sabato bila kuichafua, watu watakaofuata agano langu,


Watauliza njia ya kwenda Sayuni, na nyuso zao zikielekea huko, wakisema: Mukuje! Nao watajiunga na Yawe katika agano la milele ambalo halitasahauliwa hata kidogo.


mwenye kigongo, mutu mufupi kuliko kawaida, asiyeona sawasawa, mwenye kivimba, mwenye upele au mutu anayekuwa towashi, asikaribie kumutolea Mungu mukate wake.


Unaweza vilevile kununua watumwa kutoka kwa wageni wanaokaa pamoja nawe na jamaa zao waliozaliwa katika inchi yenu, nao watakuwa mali yako.


Wao watamwogopa sana Yawe; ataiangamiza miungu yote ya dunia. Mataifa yote katika dunia yatamwabudu; kila taifa katika pahali pake.


Wao watajiunga nawe katika kazi na kutimiza mapaswa yao kwa ukamilifu juu ya kazi zote za hema, wala kusikuwe mutu mwingine atakayekukaribia mule.


Lakini wewe peke yako na wana wako mutafanya kazi zote za kikuhani kwa ajili ya mazabahu na vyote vinavyokuwa ndani ya pazia. Hayo ni mapaswa yenu, kwa sababu ninawapa zawadi ya ukuhani. Mutu yeyote asiyestahili atakayekaribia vyombo vya hema, atauawa.


Basi Petro akaanza kuhubiri, akisema: “Sasa ninafahamu kwamba Mungu hana upendeleo,


Wamoja kati ya Wayuda wakasadiki na kujiunga pamoja na Paulo na Sila. Vilevile kundi kubwa la Wagriki walioogopa Mungu pamoja na wanawake wengi wenye heshima wakasadiki.


Halafu Paulo akaondoka pale, akaenda kukaa katika nyumba ya mutu mumoja aliyeitwa Tito Yusto, aliyekuwa mwenye kuogopa Mungu. Nyumba ya mutu huyu ilikuwa karibu sana na nyumba ya kuabudia.


kuwa mutumishi wa Yesu Kristo kwa watu wa mataifa mengine. Ninafanya kazi ya ukuhani ya kuhubiri Habari Njema ya Mungu, kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuwa kama sadaka inayokubaliwa na Mungu na iliyotakaswa na Roho Mutakatifu.


Lakini anayeungana na Bwana anageuka kuwa mumoja naye kiroho.


Kwa wakati ule mulikuwa mumetengwa mbali na Kristo. Hamukukuwa kati ya watu waliochaguliwa na Mungu, mulikuwa wageni kati yao. Ninyi hamukukuwa na pato lolote katika agano zile Mungu alizotoa katika ahadi yake kwa watu wake. Muliishi katika dunia pasipo tumaini wala kumujua Mungu.


Katika kuungana pamoja na Kristo, ninyi vilevile munaunganishwa pamoja na wengine wote kuwa makao ya Mungu kwa njia ya Roho wake.


Wazao wao, kuanzia kizazi cha tatu, wataruhusiwa kuingia katika kusanyiko la watu wa Yawe.


Barua hii inatoka kwangu mimi Petro, mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi muliochaguliwa na Mungu na ambao mulisambazwa, na munaoishi kama wakimbizi kule Ponto, Galatia, Kapadokia, Azia na Bitinia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ