“Na hata mugeni asiyekuwa Mwisraeli atakayekuja kutoka inchi ya mbali kwa ajili ya jina lako kubwa, na juu ya nguvu na ulinzi wako, akikuja kuomba katika nyumba hii,
Wayuda wakaifanya kuwa sheria kwao, kwa wazao wao na kwa mutu yeyote ambaye angejiunga nao, kwamba katika wakati uliopangwa kila mwaka, bila kukosa, siku hizo mbili zishikwe kulingana na maagizo ya Mordekayi.
Yawe atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawachagua tena Waisraeli. Atawarudisha katika inchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.
nitamupatia nafasi ya ukumbusho na ya sifa katika nyumba yangu na kuta zangu, nafasi bora kuliko kuwa na wana na wabinti. Nitamupatia jina la kukumbukwa siku zote na ambalo halitafutwa hata kidogo.
Wageni watakaoshikamana nami Yawe, kwa kunitumikia na kwa kupenda jina langu, na kuwa watumishi wangu, wote watakaoshika siku ya Sabato bila kuichafua, watu watakaofuata agano langu,
Watauliza njia ya kwenda Sayuni, na nyuso zao zikielekea huko, wakisema: Mukuje! Nao watajiunga na Yawe katika agano la milele ambalo halitasahauliwa hata kidogo.
mwenye kigongo, mutu mufupi kuliko kawaida, asiyeona sawasawa, mwenye kivimba, mwenye upele au mutu anayekuwa towashi, asikaribie kumutolea Mungu mukate wake.
Lakini wewe peke yako na wana wako mutafanya kazi zote za kikuhani kwa ajili ya mazabahu na vyote vinavyokuwa ndani ya pazia. Hayo ni mapaswa yenu, kwa sababu ninawapa zawadi ya ukuhani. Mutu yeyote asiyestahili atakayekaribia vyombo vya hema, atauawa.
Wamoja kati ya Wayuda wakasadiki na kujiunga pamoja na Paulo na Sila. Vilevile kundi kubwa la Wagriki walioogopa Mungu pamoja na wanawake wengi wenye heshima wakasadiki.
Halafu Paulo akaondoka pale, akaenda kukaa katika nyumba ya mutu mumoja aliyeitwa Tito Yusto, aliyekuwa mwenye kuogopa Mungu. Nyumba ya mutu huyu ilikuwa karibu sana na nyumba ya kuabudia.
kuwa mutumishi wa Yesu Kristo kwa watu wa mataifa mengine. Ninafanya kazi ya ukuhani ya kuhubiri Habari Njema ya Mungu, kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuwa kama sadaka inayokubaliwa na Mungu na iliyotakaswa na Roho Mutakatifu.
Kwa wakati ule mulikuwa mumetengwa mbali na Kristo. Hamukukuwa kati ya watu waliochaguliwa na Mungu, mulikuwa wageni kati yao. Ninyi hamukukuwa na pato lolote katika agano zile Mungu alizotoa katika ahadi yake kwa watu wake. Muliishi katika dunia pasipo tumaini wala kumujua Mungu.
Barua hii inatoka kwangu mimi Petro, mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi muliochaguliwa na Mungu na ambao mulisambazwa, na munaoishi kama wakimbizi kule Ponto, Galatia, Kapadokia, Azia na Bitinia.