Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 55:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Maana mawazo yangu si kama mawazo yenu, wala njia zangu si kama njia zenu. –Ni ujumbe wa Yawe.–

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 55:8
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tena jambo hili lilikuwa dogo mbele ya macho yako. Zaidi ya hayo, Bwana wangu Yawe, umeahidi kuchunga jamaa yangu kwa miaka mingi inayokuja na kunijulisha hivyo, ee Bwana wangu Yawe.


Lakini Namani alikasirika sana, akaenda zake akisema: “Nilizani kwamba hakika atanifikia na kumwomba Yawe, Mungu wake, apitishe mikono yake juu ya pahali ninapogonjwa na kuniponyesha!


Basi uangalie mbingu! Angalia mawingu yanayokuwa juu kuliko wewe!


Njia zote za Yawe ni njema na za uaminifu kwa wale wanaoshika agano lake na maagizo yake.


Mipango ya Yawe inadumu milele; kusudi lake linadumu kwa vizazi vyote.


Heri mutu anayemutumainia Yawe, mutu asiyejiunga na watu wenye majivuno, watu waliopotoka kwa kuabudu miungu ya uongo.


Ee Yawe, matendo yako makubwa yananifurahisha; nitashangilia kwa sababu ya mambo yote uliyotenda.


Njia ya mutu mwenye kosa imepotoka, lakini mwenendo wa mwenye moyo safi ni sawa.


Kama vile mbingu zinavyokuwa mbali juu na dunia mbali chini, ndivyo inavyokuwa vigumu kuelewa akili za mufalme.


Yawe wa majeshi ameapa: Kama nilivyopanga, ndivyo itakavyokuwa; kama nilivyokusudia, ndivyo itakavyokamilika.


Sisi wote tumepotea kama kondoo, kila mumoja wetu ameelekea njia yake. Lakini Yawe alimubebesha azabu, ambayo sisi wenyewe tuliistahili.


Kama ukiacha kufanya kazi siku ya Sabato, ukiacha shuguli zako siku yangu hiyo takatifu, ukiifanya siku yangu kuwa ya furaha, ukiheshimu siku hiyo takatifu ya Yawe, ukiacha shuguli zako au kupiga domo,


Muchana kutwa niliwanyooshea mikono watu waasi, watu ambao wanafuata njia zisizokuwa nzuri, watu ambao wanafuata mawazo yao wenyewe.


Ninayajua matendo yao na mawazo yao. Ninakuja kuwakusanya watu wa mataifa yote na wa luga zote, wakusanyike pamoja na kuuona utukufu wangu.


Mume akiachana na muke wake, naye muke akijiendea, na kuolewa na mwingine, mume yule anaweza kumurudilia muke huyo? Kufanya hivyo hakutaichafua inchi kabisa? Wewe Israeli, umefanya ukahaba na wapenzi wengi, sasa unataka kunirudilia mimi? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Lakini ninyi Waisraeli munasema: Anachotenda Yawe si sawa! Enyi Waisraeli, basi, ninachofanya mimi si sawa? Munachofanya ninyi ndicho kisichokuwa sawa.


Enyi watu wa Efuraimu, muko na maneno gani tena na sanamu? Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu, mimi ndiye ninayewatunza. Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi; kutoka kwangu mutapata matunda yenu.


Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ