Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 55:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Waovu waache njia zao mbaya, watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya; wamurudilie Yawe apate kuwahurumia, wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 55:7
61 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe alipoona uwingi wa uovu wa watu katika dunia, na kwamba kila kitu mwanadamu anachokusudia ndani ya moyo wake ni kiovu siku zote,


naye akatoka kwenda kukutana na mufalme Asa, akamwambia: “Unisikilize, ee Asa na watu wote wa kabila la Yuda na la Benjamina! Yawe yuko pamoja nanyi, ikiwa mutakuwa pamoja naye. Mukimutafuta, mutamupata, lakini mukimwacha, naye atawaacha.


Lakini walipopatwa na shida, walimugeukia Yawe, Mungu wa Israeli, wakamutafuta, wakamupata.


Kwa hiyo wajumbe wakapita katika inchi yote ya Israeli na ya Yuda kwa kupeleka barua zile kufuatana na amri ya mufalme na wakubwa wake. Barua hizo zilikuwa na ujumbe huu: “Enyi watu wa Israeli muliobaki nyuma ya mashambulizi ya wafalme wa Asuria. Mumurudilie Yawe, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Israeli, kusudi naye apate kuwarudilia.


Alimusihi, naye Mungu akapokea maombi yake na kusihi kwake, akamurudisha Yerusalema katika ufalme wake. Halafu Manase akatambua kwamba Yawe ndiye Mungu.


kama watu wangu hao wakijinyenyekeza, wakiomba, wakinitafuta na kuacha njia zao mbaya, basi, mimi nitawasikiliza kutokea juu mbinguni, nitawasamehe zambi yao na kustawisha inchi yao.


Ukimurudilia Mungu na kunyenyekea, ukiondoa uovu mbali na makao yako,


Lakini kwako tunapata usamehe, kusudi sisi tukuheshimu.


Ee Israeli, umutumainie Yawe, maana Yawe ni mwenye wema, naye ana nguvu kubwa ya kutukomboa.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi inayoelekea wakati nabii Natani alipomufikia kwa kumwonya juu ya uzinzi alioufanya na Batiseba.


Kama ningalikusudia maovu ndani ya moyo, Yawe hangalinisikiliza.


Anayeficha makosa yake hatafanikiwa, lakini anayeungama na kuyaacha atahurumiwa.


Mukiwa tayari kunitii, mutakula mazao mema ya inchi.


Yawe atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawachagua tena Waisraeli. Atawarudisha katika inchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.


Nami mulinzi nikajibu: Asubui inakuja, vilevile usiku; ukitaka kuuliza, uliza tu; kwenda urudi tena.


Enyi Waisraeli, mumurudilie yule muliyemwacha kabisa.


Matendo ya watu wadanganyifu ni mabaya; hao wanatunga maneno mabaya kwa kumwangamiza masikini kwa maneno ya uongo, hata kama masikini ni mwenye sheria.


Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.


Lakini mimi ndiye niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu, ndiye ninayefuta makosa kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka zambi zenu.


Nimezimisha makosa yako nayo yametoweka kama mawingu, nimefuta zambi zako, nazo zimepotea kama kunguku. Urudi kwangu maana mimi nimekukomboa.


Milima inaweza kutoweka, vilima vinaweza kuondolewa, lakini rehema zangu kwako sitaziacha, agano langu la amani litaimarishwa. Ni Yawe anayekuhurumia anayesema hivyo.


Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa muda kidogo, lakini kwa wema wa milele nitakuonea huruma. Ni Yawe Mukombozi wako anayesema hivyo.


Mafungo ninayotaka mimi ni haya: kuwafungua waliofungwa bila haki, kuziondoa kamba za utumwa, kuwaacha huru wanaogandamizwa, na kuvunja kabisa mambo yote ya kitumwa!


Muko mbio kutenda maovu, muko wepesi kumwanga damu isiyokuwa na kosa. Mawazo yenu ni mawazo ya uovu, popote munapokwenda munaacha ukiwa na uharibifu.


Murudi, enyi watoto musiokuwa na uaminifu, maana, mimi ndimi Bwana wenu. Nitawatwaa mumoja kutoka kila muji, na wawili kutoka katika kila ukoo, niwapeleke mpaka kwenye mulima Sayuni. –Ni ujumbe wa Yawe.


Ndiyo maana manyunyu yamezuizwa kuanguka, wala mvua za mwisho hazijanyesha. Hata hivyo unakausha macho kama kahaba, wala hauna haya hata kidogo.


Wewe Yerusalema, usafishe maovu ya moyo wako, kusudi upate kuokolewa. Mpaka wakati gani utaendelea kuchunga maovu?


Tupime na kuchunguza mwenendo wetu tupate kumurudilia Yawe.


Basi, uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Munirudilie, na kuacha kuziabudu sanamu zenu za miungu. Muache kufanya machukizo.


Basi, uwaambie: Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– mimi sikifurahii kifo cha mutu mwovu, lakini ninapenda mutu mwovu aachane na mwenendo wake mubaya, apate kuishi. Mugeuke, muachane na mwenendo wenu mubaya, enyi Waisraeli! Kwa nini munataka kufa?


Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!


Mungu alipoona walivyofanya, na jinsi walivyouacha uovu wao, akabadilisha nia yake, akaacha kuwatenda kama alivyokuwa amekusudia.


Mutu yeyote asikusudie kumutendea mwenzake ubaya wala musiape uongo, maana ninayachukia sana matendo hayo. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Muende kujifunza maana ya Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Ninataka huruma, lakini si sadaka zenu.’ Kwa maana sikukuja kuwaita wenye haki kunifuata, lakini watenda mabaya.”


Kwa maana ni ndani ya mutu, ni kusema ndani ya moyo wake, ndimo munamotoka mawazo mabaya yanayoleta: uzinzi, wizi, uuaji,


Maovu haya yote yanatoka ndani ya mutu, nayo yanamufanya kuwa muchafu.”


Vilevile ninawaambia, ndivyo wamalaika wa Mungu wanavyofurahi kwa ajili ya mwenye zambi mumoja anayegeuka toka zambi zake.”


Kwa sababu mwana wangu huyu alikuwa amekufa, na amefufuka, alikuwa amepotea na sasa ameonekana.’ Nao wakaanza kufurahi pamoja.


Ni kwa sababu hii ninakuambia kwamba upendo ambao mwanamuke huyu alioonyesha unahakikisha kwamba Mungu amemusamehe zambi zake zinazokuwa nyingi. Lakini yule anayesamehewa kwa machache haonyeshi upendo zaidi.”


Lakini kwanza nilihubiri wakaaji wa Damasiki, na wa Yerusalema na wa jimbo lote la Yudea nao watu wa mataifa mengine vilevile. Nilihubiri kwao kwamba wageuke toka zambi zao na kumurudilia Mungu, nao waonyeshe kwa njia ya matendo yao kwamba wamegeuka.


Basi mugeuke toka katika zambi, mumurudilie Mungu, kusudi awasamehe zambi zenu.


Halafu ile tamaa mbaya ikisha kukomaa, inazaa zambi, nayo zambi ikisha kukomaa inazaa lufu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ