Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 55:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ee ninyi wote wenye kiu mukuje kwenye maji! Mukuje, wote hata musiokuwa na feza; mununue chakula na mupate kula, mununue divai na maziwa. Bila feza, bila malipo!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 55:1
39 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninakunyooshea mikono yangu. Ninakuhitaji wewe, kama inchi kavu inavyohitaji mvua.


Zaburi ya Daudi wakati alipokuwa katika jangwa la Yudea.


“Enyi watu wote, ninawaita ninyi! Wito wangu ni kwa ajili ya wanadamu.


Hekima amejenga nyumba yake, nyumba yenye nguzo saba.


“Kuja ukule chakula, na ukunywe divai niliyotengeneza.


Heri midomo yako ingalinibusu, maana mapendo yako ni bora kuliko divai.


Unipeleke, tuende haraka, mufalme amenileta katika chumba chake. Tutafurahi na kukushangilia pamoja, tutasifu mapenzi yako kuliko divai. Wabinti wana haki ya kukupenda!


Ninaingia katika bustani yangu, dada yangu, muchumba wangu. Ninakusanya manemane na majani yenye harufu, ninakula sega langu la asali, ninakunywa divai yangu na maziwa yangu. Mukule, enyi warafiki, mukunywe; mukunywe sana, wapendwa wangu.


Mukiwa tayari kunitii, mutakula mazao mema ya inchi.


Nitaimwangilia maji inchi yenye kiu, na kutiririsha muto katika inchi iliyokauka. Nitajaza roho wangu juu ya wazao wako, nitawamwangia watoto wako baraka yangu.


Yawe anasema hivi: Ninyi muliuzishwa bure bila malipo yoyote, na mutakombolewa bila kulipa feza.


Maji yetu tunayapata kwa feza, kuni zetu kwa kuzinunua.


Yule mutu akanirudisha kwenye kiingilio cha hekalu. Huko, maji yalikuwa yakitoka chini ya kizingiti cha hekalu kuelekea upande wa mashariki, (kwa maana hekalu lilielekea upande wa mashariki). Maji yalikuwa yakitiririka kutoka chini ya upande wa kusini wa mulango wa hekalu, upande wa kusini wa mazabahu.


Kila pahali muto huu utakapopita, kutaishi aina zote za nyama na samaki. Muto huu utayafanya maji ya bahari ya Chumvi kuwa maji baridi. Kokote utakakopita utaleta uzima.


Inchi ya Asuria haitatuokoa, hatutategemea tena farasi wa vita. Hatutaziita tena Mungu wetu hizo sanamu tulizochonga. Kwako, ee Mungu, yatima anapata huruma.


Watu wa Efuraimu watakuwa kama mashujaa katika vita; watajaa furaha kama watu waliokunywa divai. Watoto wao wataona hayo na kufurahi, watajaa furaha ndani ya moyo kwa sababu yangu mimi Yawe.


Basi, nikamwuliza: Unakwenda wapi? Naye akanijibu: Ninakwenda kuupima urefu na upana wa Yerusalema.


Yawe wa majeshi atawalinda watu wake, nao watawaangamiza waadui zao. Watapiga kelele katika vita kama walevi, wataimwanga damu ya waadui zao. Itatiririka kama damu ya nyama wanaotolewa kwa sadaka iliyomiminwa juu ya mazabahu kutoka ndani ya bakuli.


Muponyeshe wagonjwa, mufufue wafu, mutakase wenye ukoma, mufukuze pepo. Mulipokea bure, mutoe bure vilevile.


“Ufalme wa mbinguni unafanana na mali iliyofichwa katika shamba moja. Mutu mumoja alipoiona, akaificha tena. Halafu kwa furaha kubwa akaenda kuuzisha vitu vyake vyote na kununua lile shamba.


Nami ninawaambia kwamba tangia sasa sitakunywa tena divai mpaka siku ile nitakapoikunywa mupya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”


Heri wale wanaokuwa na njaa na kiu ya kufanya yanayokuwa haki, maana watashibishwa!


Lakini Petro akamujibu: “Feza yako ipotelee mbali pamoja nawe, kwa sababu umezani kwamba unaweza kununua ile zawadi ya Mungu kwa njia ya feza!


Lakini kwa neema ya Mungu wanahesabiwa haki kwa bure kwa njia ya Kristo Yesu anayewakomboa.


Niliwakunywesha maziwa, sikuwapa chakula kigumu, kwa maana mulikuwa hamujakiweza bado. Na hata sasa hamukiwezi,


Kama vile watoto wachanga wanaotamani maziwa, na ninyi vilevile mukuwe na hamu ya kunywa maziwa safi ya kiroho, kusudi mupate kukomaa na kuokolewa.


Akasema tena: “Sasa ni mwisho! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Yule anayesikia kiu, nitamupa maji ya kunywa yanayotoka katika chemichemi ya maji ya uzima pasipo kulipa.


Kisha yule malaika akanionyesha muto wa maji ya uzima wenye kungaa kama kioo, uliokuwa ukitiririka toka kwenye kiti cha kifalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo.


Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.


Kwa hiyo ninakushauria kununua kwangu zahabu iliyosafishwa kwa moto, kusudi upate kuwa tajiri. Vilevile ununue nguo nyeupe, upate kuvaa na kufunika uchi wako unaokuletea haya. Tena ununue dawa ya kutia ndani ya macho yako, kusudi upate kuona.


Boazi akakwenda kwa nafasi ya kufanyia mukutano kule kwenye mulango wa muji, akaikaa chini. Kisha yule ndugu ya Elimeleki ambaye Boazi alikuwa amemutaja, akapita karibu na pale. Boazi akamwita, akasema: “Kuja, uikae hapa ndugu.” Basi yule mutu akakuja na kuikaa pale.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ