mapazia ya upango, nguzo zake na vikalio vyake; pazia la mulango wa upango, kamba zake na misumari yake; vyombo vyote vilivyohitajika katika kazi ya hema takatifu, ni kusema hema la mukutano;
Muangalie Sayuni tunamofanyia sikukuu zetu; muangalie Yerusalema, makao matulivu, hema imara; misumari yake haitaongolewa hata kidogo, kamba zake hazitakatwa hata moja.
Lakini hema yangu imebomolewa, kamba zake zote zimekatika; watoto wangu wameniacha, na kujiendea, wala hawako tena; hakuna wa kunisimikia tena hema yangu, wala wa kunitundikia mapazia yangu.