Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 54:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Silaha zote zilizotengenezwa kwa kukuzuru wewe hazitafaa kwa kitu chochote. Mutu akikushitaki, utamushinda. Hiyo ndiyo haki niliyowapangia watumishi wangu. Hizo ndizo haki nilizowahakikishia. –Ni ujumbe wa Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 54:17
44 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini sasa, unyooshe mukono wako uguse mali yake. Utaona namna atakutukana waziwazi!”


Lakini sasa, unyooshe mukono wako umuguse mwili wake. Utaona namna atakutukana waziwazi.”


Yawe alipomaliza kuongea na Yobu, akamwambia Elifasi wa inchi ya Temani: “Kasirani yangu imewaka juu yako na warafiki zako wawili maana hamukusema ukweli juu yangu kama vile mutumishi wangu Yobu alivyofanya.


Kwa hiyo, kila mwaminifu akutolee maombi wakati wa taabu. Mafuriko ya maji hayatamufikia.


Ninaomba nikae katika nyumba yako milele, nipate kukimbilia chini ya mabawa yako.


Nitataja matendo yako makubwa, ee Bwana wangu Yawe; nitatangaza kwamba wewe ndiwe mwenye haki.


Nguvu na haki yako, ee Mungu, vinafika mpaka juu katika mbingu. Wewe umefanya mambo makubwa sana. Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe?


Aha! Ngurumo ya watu wengi! Wananguruma kama bahari. Aha! Mulio wa watu wa mataifa! Yanatoa mulio kama wa maji mengi.


Mufungue milango ya muji, taifa aminifu liingie; taifa linalotenda mambo ya haki.


Mataifa yote yanayoshambulia Yerusalema yatakuwa kama mutu mwenye njaa anayeota ndoto kwamba anakula lakini anaamuka angali bado na njaa, na kama mutu mwenye kiu anayeota kwamba anakunywa lakini anaamuka muzaifu, na angali bado na kiu.


Muwaambie watu wa haki jinsi wanavyokuwa na heri, maana watakula matunda ya matendo yao.


Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.


Kweli! Wote waliokukasirikia, watapata haya na kufezeheka. Wote wanaopingana nawe, watakuwa wa bure na kuangamia.


Siku ya kuwakomboa inakaribia, haiko mbali tena; siku ya kuwaokoa ninyi haitachelewa. Nitauokoa Sayuni, nitaleta utukufu kwa Israeli.


Muteteaji wangu yuko karibu. Ni nani atakayepingana nami? Akuje tusambe naye. Adui yangu ni nani? Ajitokeze mbele basi.


Angalia Bwana wetu Yawe ananisaidia. Ni nani anayeweza kusema niko na kosa? Waadui zangu wote watachakaa kama nguo, nondo watawatafuna.


Ukombozi wangu unakaribia upesi; wokovu nitakaoleta unaanza kutokea. Mimi mwenyewe nitayatawala mataifa. Wakaaji wa inchi za mbali wananingojea, wanaitegemea nguvu yangu.


Mutu yeyote akikuja kukushambulia, hatakuwa ametumwa nami. Yeyote atakayekushambulia, ataangamia mbele yako.


Mimi ndiye niliyemwumba mufuaji wa vyuma, anayewasha moto wa makaa na kufua silaha. Ni mimi vilevile niliyemwumba mwangamizaji anayeangamiza.


utapata furaha yako kwangu mimi Yawe, nitakupatia ushindi katika kila upinzani katika inchi, nitakulisha mali ya Yakobo, babu yako. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.


Watu wako wote watakuwa wa haki, nao watarizi inchi milele. Hao ni chipukizi nililopanda mimi, kazi ya mikono yangu kwa ajili ya utukufu wangu.


Nitafurahi sana kwa sababu ya Yawe, nafsi yangu itashangilia kwa sababu ya Mungu wangu. Maana amenivalisha nguo ya wokovu, amenifunika kanzu ya haki, kama bwana arusi anavyojipamba kwa shada la maua, kama bibi arusi anavyojipamba kwa ushanga wake.


Katika siku za utawala wake, inchi ya Yuda itaokolewa na inchi ya Israeli itakuwa katika usalama. Naye ataitwa kwa jina la Yawe Ni Haki Yetu.


Basi, mufalme Nebukadneza akaukaribia mulango wa furu la moto mukali, akaita: Sadiraki, Mesaki na Abedenego, watumishi wa Mungu Mukubwa, mutoke mukuje hapa! Sadiraki, Mesaki na Abedenego wakatoka ndani ya moto.


Ilipokuwa asubui mapema, mufalme Dario aliamuka, akaenda kwa haraka kwenye pango la simba.


Nami sasa ninakuambia: ewe Petro, wewe ni jiwe, na juu ya jiwe hili, nitajenga musingi wa kanisa langu, na hata uwezo wa lufu hautaweza kulishinda.


Kwa maana kwa njia ya Kristo, Sheria imepata kufikia ukomo wake kusudi kila mutu anayeamini apate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.


kuhesabiwa haki na Mungu kunapatikana kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote wanaoamini, kwa maana hakuna tofauti yoyote kati yao,


Basi sasa hakuna azabu kwa wale wanaoungana na Yesu Kristo.


Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


na kuungana naye kabisa. Nami sihesabiwi haki tena kufuatana na mambo niliyofanya, ndiyo ile haki inayopatikana kwa njia ya kushika Sheria. Lakini ninahesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Kristo, ndiyo ile haki inatoka kwa Mungu, naye anamuhesabia haki yule anayeamini.


Lakini mimi sikumusikiliza Balama, naye akawabariki, nami nikawaokoa ninyi toka mikono ya Balaka.


Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.


Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni, ikisema: “Sasa wokovu, uwezo na ufalme wa Mungu, na mamlaka ya Kristo wake vimefika. Ni vile, kwa yule aliyekuwa akiwashitaki wandugu zetu mbele ya Mungu wetu muchana na usiku ametupwa chini ya mbingu.


Yonatani akamwambia: “Usiogope, baba yangu Saulo hatakupata. Wewe utakuwa mufalme wa Israeli, mimi nitakuwa wa pili wako. Hata Saulo baba yangu anajua jambo hili.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ