Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 54:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Ewe Yerusalema, uliteseka, ulitaabishwa na kukosa wa kukufariji, lakini nitakujenga upya kwa mawe ya bei kali, misingi yako itakuwa ya mawe ya yakuti.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 54:11
43 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Unajua kwamba baba yangu Daudi hakuweza kumujengea Yawe, Mungu wake, hekalu la kumwabudia, kwa sababu ya vita vilivyomuzunguka pande zote mpaka hapo Yawe alipomupatia ushindi.


Aliipakaa zahabu kwenye sakafu ya vyumba vya ndani na vya inje.


Basi nimejitia kwa kadiri ya uwezo wangu wote kwa kuwekea nyumba ya Mungu wangu, akiba ya zahabu ya kutengeneza vitu vya zahabu, feza ya kutengeneza vitu vya feza, shaba ya kutengeneza vitu vya shaba, chuma cha kutengeneza vitu vya chuma, na miti ya kutengeneza vitu vya miti. Zaidi ya hayo, nimetayarisha kwa wingi mawe ya rangi na mawe ya kupamba, mawe ya kuchorwa, mawe ya bei kali ya kila namna na marumaru.


Mufalme Solomono aliipamba nyumba ya Yawe kwa mawe mazuri ya bei kali. Zahabu aliyotumia ilitoka katika inchi ya Parawaimu.


Haiwezi kupimwa kwa zahabu ya Ofiri, wala kwa mawe ya sardoniki au ya yakuti samawi.


Yawe ni karibu na wenye kuvunjika moyo; anawaokoa wote waliokata tamaa kabisa.


Nyuma ya muda murefu, mufalme wa Misri akakufa. Waisraeli wakaugua na kulia kutokana na hali yao ya utumwa na kilio chao kikamufikia Mungu juu.


wakamwona Mungu wa Israeli. Chini ya miguu yake kulikuwa kitu kama sakafu ya mawe ya yakuti samawi, kikiwa safi kama mbingu inayoangaa.


Basi, malaika wa Yawe akamutokea katika mwali wa moto katikati ya kichaka. Musa akaangalia, akashangaa kuona kichaka kinawaka moto na wala hakiungui.


Kisha Yawe akamwambia: “Nimeona mateso ya watu wangu wanaokuwa katika inchi ya Misri na nimesikia kilio chao kinachosababishwa na watesaji wao. Ninajua mateso yao,


Mikono yake ni kama pete za zahabu, amevaa mawe ya bei kali. Kiwiliwili chake ni kama pembe za tembo zilizopambwa kwa mawe ya yakuti ya rangi ya samawi.


Basi watapewa jibu gani wajumbe wa taifa hilo? Wataambiwa: Yawe ameijenga imara Sayuni, na wamasikini kati ya watu wake watakimbilia kule.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninaweka katika Sayuni jiwe la musingi, jiwe ambalo limeimarishwa. Jiwe la pembe, la bei kali, jiwe ambalo ni la musingi imara; jiwe linalokuwa na maandiko haya: Anayeamini hataanguka.


Ndimi ninasema juu ya mufalme Kiro: Ni muchungaji niliyemuchagua kwa ajili yangu. Yeye atatimiza mipango yangu yote. Ndimi ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema utajengwa tena upya; na juu ya hekalu: Musingi wako utawekwa tena.


Wewe Sayuni unasema: Yawe ameniacha. Hakika Bwana wangu amenisahau.


Basi, sikiliza, ewe Yerusalema unayeteseka; sikiliza wewe uliyelewa, lakini sio kwa divai.


Nami nitakitia katika mikono ya wanaokutesa, waliokuambia ulalie tumbo wapite juu yako, nawe ukaufanya mugongo wako kama vile udongo wa njia, kama vile barabara ya kupitia.


Minara yako nitaijenga kwa mawe ya akiki, milango yako kwa almasi, na ukuta wako kwa mawe ya bei kali.


Yerusalema, Yawe amekuita tena. Ulikuwa kama vile muke aliyeachwa na kuhuzunika. Mungu wako anasema: Muke aliyeolewa akiwa kijana, anaweza kuachiliwa?


Wewe ulikuwa umeachwa na kuchukiwa, hakuna aliyependa hata kupita ndani yako. Lakini sasa nitakufanya ukuwe na utukufu milele, utakuwa muji wa furaha kwa kizazi na kizazi.


Sasa wanakuita wewe Sayuni: “Aliyetupiliwa”, “Muji usioshugulikiwa na mutu”. Lakini nitakurudishia afya yako, nitaponyesha vidonda vyako. –Ni ujumbe wa Yawe.


Sikiliza ninavyolalamika; hakuna wa kunifariji. Waadui zangu wote wamesikia juu ya taabu yangu: wanafurahi kwamba umeniletea hasara. Uifanye ile siku uliyoahidi ifike, uwafanye nao wateseke kama mimi.


Juu ya kitu hicho niliona kitu kimoja kinachofanana na kiti cha kifalme chenye rangi la jiwe la yakuti. Juu yake kulikuwa kunaikaa kitu kinachofanana na mutu.


Kisha nikaona kwamba katika lile anga juu ya vichwa vya makerubi kulikuwa kitu kinachofanana na jiwe la rangi ya samawi, umbo lake kama kiti cha kifalme.


Siku inakuja ambapo kuta za muji wenu zitajengwa upya. Siku hiyo mipaka ya inchi yenu itapanuliwa.


Mara moja zoruba kubwa ikatokea katika ziwa na maji yakajitupatupa ndani ya chombo. Lakini Yesu alikuwa amelala usingizi.


Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”


Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


Ninyi vilevile ni kama jengo linalosimama juu ya musingi uliowekwa na mitume na manabii; Yesu Kristo mwenyewe ndiye jiwe kubwa la pembe.


Hapo hasira yangu itawawakia siku hiyo, nami nitawaacha na kuficha uso wangu mbali nao, wataangamizwa. Maovu mengi na taabu zitawapata hata watambue kwamba maovu hayo yamewapata kwa sababu Mungu wao hayuko kati yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ