Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 54:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Milima inaweza kutoweka, vilima vinaweza kuondolewa, lakini rehema zangu kwako sitaziacha, agano langu la amani litaimarishwa. Ni Yawe anayekuhurumia anayesema hivyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 54:10
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hivi ndivyo jamaa yangu inavyokuwa mbele ya Mungu. Maana amefanya nami agano la kudumu milele; agano kamili na lenye kuwa imara. Naye atanifanikisha katika mahitaji yangu yote.


Wewe uliumba dunia tokea zamani, mbingu ni kazi ya mikono yako.


Mungu ni kimbilio letu na nguvu yetu; yeye ni musaada wetu wakati wa taabu.


Kwa hiyo hatutaogopa kitu chochote, hata dunia ikiyeyuka na milima kutikisika kutoka bahari,


Hawatasikia tena njaa wala kuwa na kiu. Upepo wenye kuunguza wala jua havitawachoma, mimi niliyewahurumia nitawaongoza na kuwapeleka kwenye chemichemi za maji.


Lakini Yawe anasema: Munafikiri kwamba mama anaweza kumusahau mutoto anayemunyonyesha, wala kumuchukia mutoto wa tumbo lake? Hata kama mama anaweza kumusahau mutoto wake, mimi sitakusahau hata kidogo.


Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa muda kidogo, lakini kwa wema wa milele nitakuonea huruma. Ni Yawe Mukombozi wako anayesema hivyo.


Mutatoka Babeli kwa furaha; mutaongozwa muende kwa amani. Milima na vilima mbele yenu vitapiga kelele na kuimba, na miti yote katika mashamba itawapigia mikono.


Mutege sikio, enyi watu wangu, mukuje kwangu; munisikilize, kusudi mupate kuishi. Nami nitafanya nanyi agano la milele; nitawatendea mema niliyomwahidi Daudi.


Waovu waache njia zao mbaya, watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya; wamurudilie Yawe apate kuwahurumia, wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.


Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.


Mimi Yawe ninapenda watu wafuate sheria yangu; ninachukia unyanganyi na uovu. Nitawatunza watu wangu kwa uaminifu, nitafanya nao agano la milele.


Nitakumbusha mema ya Yawe, sifa za Yawe, matendo yake yote kwetu, mambo mazuri aliyowatendea Waisraeli, rehema yake, na wingi wa wema wake.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Ikiwa itanifikia kuvunja mipango ile, halafu nitaweza vilevile kukomesha kizazi cha Waisraeli, wasiitwe tena taifa langu siku zote. –Ni ujumbe wa Yawe.


Yawe anasema hivi: Kama munaweza kuvunja agano langu nililofanya na usiku na muchana kwa jinsi usiku na muchana visikuwe kwa wakati wake,


Hivi, kasirani yangu itatosheka juu yako, wivu niliokuwa nao juu yako utakwisha; nitatulia wala sitaona hasira tena.


Nitafanya nao agano la amani. Nitaondoa nyama wakali katika inchi, kusudi kondoo wangu wakae katika mbuga kwa usalama na kulala katika pori.


Katika agano hilo, niliwaahidi uzima na amani na kwamba wao wanapaswa kunitii mimi, nao kwa upande wao walinitii mimi na kuogopa jina langu.


Kwa hiyo umwambie kwamba ninafanya naye agano la amani.


Nami sasa ninakuambia: ewe Petro, wewe ni jiwe, na juu ya jiwe hili, nitajenga musingi wa kanisa langu, na hata uwezo wa lufu hautaweza kulishinda.


Mbingu na dunia vitatoweka, lakini maneno yangu hayatabadilika hata kidogo.


Kweli ninawaambia: kwa muda wote mbingu na dunia vitakapokuwa vingali, hakuna hata herufi moja wala nukta moja ya Sheria itakayoondoshwa mpaka yote yatimie.


Kwa maana Mungu habadilishi mafikiri juu ya zawadi anazotoa, wala juu ya wale anaowachagua.


alituokoa sisi. Hakufanya vile kwa sababu ya matendo yetu ya haki, lakini alituokoa kwa sababu ya huruma yake kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetuwezesha kuzaliwa mara ya pili na kuwa na maisha mapya kwa kutusafisha kwa maji.


Neno hili “mara moja tena” linaonyesha kwamba vitu vilivyoumbwa vitatikiswa na kutoweka, kusudi vile visivyoweza kutikiswa vipate kudumu.


Mbingu zikaviringwa na kuwa kama kizingo cha karatasi na kutoweka. Milima yote na visanga vyote vikahamishwa kutoka kwenye nafasi yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ