Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 54:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe anasema hivi: Imba kwa shangwe, ewe unayekuwa tasa, wewe ambaye haujapata kuzaa! Piga kelele na kuimba kwa nguvu, wewe usiyepata kuzaa mutoto. Maana watoto wako wewe uliyeachwa watakuwa wengi kuliko wa yule anayekuwa na mume.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 54:1
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye Sara akasema: “Mungu amenipatia kicheko; yeyote atakayesikia habari hizi, atacheka pamoja nami.”


Anamurudishia heshima mwanamuke anayekuwa tasa; anamufurahisha kwa kumujalia watoto. Haleluia!


Tuna dada mudogo, ambaye bado hajaota maziba. Basi, tutamufanyia dada yetu nini siku atakapochumbiwa?


Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.


Watu wanalalamika, wanaimba kwa shangwe. Kutoka upande wa magaribi, wanatangaza ukubwa wa Yawe,


Muimbe kwa furaha enyi mbingu, kwa sababu ya yale Yawe aliyotenda. Mupige kelele enyi vilindi vya dunia! Mupige vigelegele enyi milima! Enyi mapori na miti yote inayokuwa ndani yake, mushangilie. Maana Yawe amewakomboa wazao wa Yakobo, naye atatukuzwa katika inchi ya Israeli.


Muimbe kwa furaha, enyi mbingu! Ushangilie ewe dunia, Enyi milima, mulalamike kwa furaha, maana Yawe amewafariji watu wake, anawaonea huruma watu wake wanaoteseka.


Kweli umepatwa na uharibifu, makao yako yamekuwa matupu, na inchi yako imeteketezwa. Lakini sasa itakuwa ndogo sana kwa wakaaji wake.


Watoto wako waliozaliwa katika uhamisho, watakulalamikia wakisema: Inchi hii ni ndogo sana; utupatie nafasi zaidi ya kuishi.


Hautaitwa tena: Aliyeachwa, wala inchi yako haitaitwa: “Ukiwa”. Lakini utaitwa: “Ninamufurahia”, na inchi yako itaitwa: “Aliyeolewa”. Maana Yawe amependezwa nawe, naye atakuwa kama mume wa inchi yako.


Muji wangu mutakatifu, ni kama mama anayezaa bila kupata uchungu; mbele ya uchungu kuanza, amekwisha zaa mutoto.


Imba kwa sauti, ewe Sayuni, piga vigelegele, ee Israeli. Furahi na kushangilia kwa moyo wote, ewe Yerusalema!


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Ufurahi wewe tasa, ushangilie, upige kelele wewe usiyejua uchungu wa kuzaa. Kwa maana muke aliyeachwa na mume, atakuwa na watoto wengi kuliko yule anayekuwa naye.”


Wale ambao zamani walikuwa na chakula tele, sasa wanafanya kazi wapate chakula. Lakini waliokuwa na njaa, sasa hawana njaa tena. Mwanamuke tasa, amezaa watoto saba. Lakini mama mwenye watoto wengi, sasa ameachwa bila mutoto.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ