Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 53:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Lakini aliumizwa kwa sababu ya zambi zetu, alipondwa kwa sababu ya maovu yetu. Kwa kuazibiwa kwake sisi tumepata uzima; kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 53:5
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”


Yule malaika anaweza kumwonea huruma na kumwomba Mungu: “Umwokoe asiingie katika shimo; nimepata ukombozi wake.”


Ninakutukuza, ee Yawe, maana umeniokoa, wala haukuwaacha waadui zangu wanisimange.


Mapigo yanayoumiza ni dawa ya kuondoa uovu; fimbo inasafisha nafsi mpaka ndani kabisa.


Museme na watu wa Yerusalema kwa upole, muwaambie kwamba utumwa wao umekwisha, wamesamehewa uovu wao. Yawe amewaazibu mara mbili kwa sababu ya zambi zao zote.


Niliona mwenendo wao, lakini nitawaponyesha; nitawaongoza na kuwapa faraja, nitawatuliza hao wanaoomboleza.


Naye akinigusa nalo kwenye mudomo, akasema: Kaa hili limekugusa kwenye mudomo; umeondolewa kosa lako, umesamehewa zambi yako.


Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


Kwa maana Mwana wa Mutu hakukuja kutumikiwa, lakini kutumikiana na kutoa maisha yake kusudi awakomboe watu wengi.”


Alitolewa kufa sababu ya makosa yetu na kufufuliwa kusudi tupate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu.


Kwanza nimewatolea mafundisho haya ambayo mimi mwenyewe nilipokea: Kristo alikufa kwa sababu ya zambi zetu kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema.


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.


Mufikiri kwa uangalifu, kwa sababu ya watoto wenu ambao hawakujua wala hawakuona azabu ya Yawe, uwezo wake na nguvu zake,


Na kwa sababu Yesu Kristo alifanya mapenzi ya Mungu, sisi tumetakaswa zambi kwa njia ya mwili wake alioutoa sadaka kwa mara moja tu.


Kwa maana kwa njia ya sadaka moja aliyotoa, amewafanya wale aliowatakasa kuwa wakamilifu hata milele.


Ijapokuwa alikuwa Mwana wa Mungu, alijifunza kutii kwa njia ya mateso yale aliyopata.


Hivi vilevile Kristo naye alijitoa kufa mara moja kusudi aondoe zambi za watu wengi. Naye atarudi tena, si kwa ajili ya kuondoa zambi, lakini kwa kuwaokoa wale wanaomungojea.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ