Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 53:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Yawe alipenda kumuponda kwa mateso. Alitoa uzima wake kwa ajili ya kuondoa zambi. Mutumishi wa Mungu atakuwa na wazao; ataishi maisha marefu. Yeye ndiye atakayetimiza mupango wa Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 53:10
62 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wako watajitolea, siku utakapokwenda kuwapiga waadui. Juu ya milima mitakatifu vijana wako watakufikia, kama umande unaotokeza asubui mapema.


lakini anapendezwa na watu wanaomuheshimu, ndio wanaotegemea wema wake.


Maana Yawe anapendezwa na watu wake; yeye anawaheshimisha wanyenyekevu kwa kuwapa ushindi.


Umemufikia, ukamupatia baraka nzurinzuri; umemuvalisha taji ya zahabu safi juu ya kichwa chake.


Wenye kiburi wote katika dunia watamwabudu; wote ambao ni wa kufa watainama mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uzima wao.


Vizazi vyao vitamutumikia; watu wataelezea kizazi kinachokuja habari za Yawe,


Kambi zao ziachwe matongo, mutu yeyote asiishi katika mahema yao.


Jina la mufalme litukuzwe siku zote; utukufu wake udumu muda wote jua litakapokuwa. Kwake mataifa yote yabarikiwe; watu wote wamwite mwenye heri!


Haki istawi maisha yake yote, na amani kwa wingi mpaka mwezi ukome.


Nitamwonyesha wema wangu kwa milele, na agano langu kwake litadumu siku zote.


“Nimeapa mara moja tu kwa utakatifu wangu; nami sitamwambia Daudi uongo.


Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


Nilitangaza mambo ya mwisho tangu mwanzo, tangu zamani nilitangaza mambo yatakayotukia. Kusudio langu litatimia; mimi nitatimiza nia yangu yote.


Lakini mimi nikafikiri: Nimeshugulika bure, nimetumia nguvu zangu bure kabisa. Hata hivyo, Yawe atanipa haki yangu; mushahara wa kazi yangu uko kwa Mungu.


Kwa hiyo nitamugawanyia sehemu pamoja na wakubwa, atagawanya vitu vilivyotekwa pamoja na wenye nguvu. Alijitoa yeye mwenyewe hata kufa; aliwekwa kundi moja na watu wakosaji. Alizibeba zambi za watu wengi, akawaombea musamaha hao wakosaji.


maana utapanuka kila upande; wazao wako watarizi mataifa, miji iliyokuwa ukiwa itajaa watu.


Wazao wao watajulikana kati ya mataifa; watajulikana kati ya watu wengine. Kila mutu atakayewaona atakubali kwamba wao ni watu waliobarikiwa na Yawe.


Kama vile mbingu mupya na dunia mupya nitakazoumba zitakavyodumu milele kwa uwezo wangu, ndivyo wazao wako na jina lako litakavyodumu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Nitafurahi kuwatendea mema; nitawasimika siku zote katika inchi hii na kuwatendea kwa uaminifu.


Basi, uwaambie: Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– mimi sikifurahii kifo cha mutu mwovu, lakini ninapenda mutu mwovu aachane na mwenendo wake mubaya, apate kuishi. Mugeuke, muachane na mwenendo wenu mubaya, enyi Waisraeli! Kwa nini munataka kufa?


Watakaa katika inchi ya wazee wao ambayo nilimupa Yakobo. Wao na watoto wao na wajukuu wao wataishi humo milele. Naye Daudi, mutumishi wangu, atakuwa mutawala milele.


Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


Yawe, Mungu wako, yuko pamoja nawe. Yeye ni shujaa anayekuletea ushindi. Yeye atakufurahia kwa furaha kubwa. Kwa upendo wake atakujalia uzima mupya. Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Yeye atatawala taifa la Israeli hata milele, nao ufalme wake hautakuwa na mwisho.”


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Kweli, kweli, ninawaambia: punje ya ngano inabaki peke yake tu, isipokuwa kama yenye kufa na kuzikwa ndani ya udongo. Lakini kama ikiwa yenye kufa, inatoa matunda mengi.


Na ikiwa Mungu ametukuzwa kwa njia yake, basi Mungu vilevile atamutukuza Mwana kwa njia yake mwenyewe, naye atamutukuza bila kukawia.


Kwa maana tunajua kwamba Kristo amefufuliwa, naye hawezi kufa tena, kwa sababu kifo hakina tena uwezo juu yake.


Yeye hakumwacha Mwana wake wa pekee, lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote. Namna gani atakosa kutupatia vilevile vitu vyote kwa njia ya mwana wake?


Watu wanaotawaliwa na hali ya kimwili hawawezi kumupendeza Mungu.


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”


Mungu amekusudia tangu zamani kutukubali sisi kuwa watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Alifanya vile kufuatana na mapenzi yake.


Ametujulisha mipango yake iliyokuwa imefichwa; ndiyo ile aliyokusudia kwa mapenzi yake tangu mbele kwamba ataitimiza kwa njia ya Kristo.


Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.


Kwa sababu hii tunawaombea siku zote kusudi Mungu wetu awawezeshe kustahili kuishi kufuatana na mwito wake. Tunaomba kwamba kwa uwezo wake atimize nia zenu zote njema na kukamilisha kazi yenu ya imani.


Tena anasema: “Nitamutumainia Mungu.” Na tena anasema: “Mimi ni hapa pamoja na watoto Mungu alionipatia.”


Yeye hahitaji kutoa sadaka kila siku kama vile Makuhani wengine Wakubwa, kwanza kwa ajili ya zambi zake mwenyewe na kisha kwa ajili ya zambi za watu. Kwa maana amefanya vile mara moja tu wakati alipojitoa mwenyewe kufa.


Ikiwa ni hivi, damu ya Kristo haitakuwa na uwezo zaidi wa kututakasa? Kwa maana kwa njia ya Roho anayeishi kwa milele, Kristo alijitoa mwenyewe kwa Mungu kuwa sadaka kamilifu. Nayo damu yake ikazitakasa zamiri zetu toka katika matendo yasiyofaa, kusudi tupate kumutumikia Mungu Mwenye Uzima.


Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.


Mimi ni mwenye uzima. Nilikuwa nimekufa, lakini sasa mimi niko muzima kwa milele na milele. Niko na mamlaka juu ya lufu na kuzimu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ