Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 52:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Sikiliza sauti ya walinzi wako; wanaimba pamoja kwa furaha, maana wanaona kwa macho yao wenyewe kurudi kwa Yawe katika Sayuni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 52:8
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu watatangaza jina la Yawe kule Sayuni; sifa zake zitatangazwa kule Yerusalema,


Walinzi wa muji waliniona walipokuwa wanazunguka katika muji. Basi nikawauliza: Mumemwona mupenzi wangu wa moyo?


Walinzi wa muji walinikuta, walipokuwa wakizunguka katika muji. Wakanipiga na kuniumiza; nao walinzi wa mulango wakaninyanganya ushungi wangu.


Watu wanalalamika, wanaimba kwa shangwe. Kutoka upande wa magaribi, wanatangaza ukubwa wa Yawe,


Siku ile watu wataimba wimbo huu katika inchi ya Yuda: Sisi tuna muji imara: Mungu anatulinda kwa kuta na upango.


Siku hiyo, muimbe juu ya shamba zuri la mizabibu:


Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwangaza wa jua utakuwa mara saba ya mwangaza wake wa kawaida, sawa vile kwamba mwangaza wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Yawe atakapofunga vidonda na kuponyesha mapigo aliyowaletea watu wake.


Waliokombolewa na Yawe watarudi, watakuja Sayuni wakipiga vigelegele. Watakuwa wenye furaha ya milele, watajaliwa furaha na shangwe; huzuni na kilio vitatoweka kabisa.


Kwenda juu ya mulima murefu, ewe Sayuni, utangaze habari njema. Lalamika kwa nguvu, ewe Yerusalema, utangaze habari njema. Lalamika bila kuogopa. Uambie miji ya Yuda: Muangalie: Mungu wenu!


Sasa, muondoke Babeli! Mukimbie kutoka kwa Wakaldea! Mutangaze jambo hili kwa sauti za shangwe. Mueneze habari zake kila pahali katika dunia. Museme: Yawe amekomboa taifa la mutumishi wake Yakobo.


Maana walinzi wa Israeli wote ni vipofu; wote hawana akili yoyote. Wote ni kama imbwa bubu wasioweza kufoka, wanalala tu na kuota ndoto, wanapenda sana kusinzia!


Yawe anasema: Piga kelele, wala usijizuize; ulalamike kwa sauti kubwa kama baragumu. Uwatangazie watu wangu makosa yao, uwaambie wazao wa Yakobo zambi zao.


Juu ya kuta zako, ee Yerusalema, nimeweka walinzi, usiku na muchana hawatakaa kimya hata kidogo. Enyi munaomukumbusha Yawe ahadi yake, musikae kimya;


Watakuja na kuimba kwa sauti juu ya mulima Sayuni, watapata utukufu juu ya wema wangu mimi Yawe, kwa ajili ya ngano, divai na mafuta ninavyowapa, kwa ajili ya kondoo na ngombe vilevile; maisha yao yatakuwa kama bustani iliyotiliwa maji, wala hawataregea tena.


Nitawapa moyo mumoja na nia moja, wapate kuniheshimu mimi siku zote, kwa faida yao wenyewe na kwa faida ya watoto wao watakaofuata.


sauti za arusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wanaleta sadaka za shukrani katika nyumba ya Yawe. Wataimba hivi: Mumushukuru Yawe wa majeshi kwa sababu Yawe ni muzuri, kwa maana wema wake unadumu milele. Nitairudishia inchi hii hali yake ya zamani. –Ni Yawe anayesema.


Nitawastawisha tena Wayuda na watu wa Israeli; nitawaimarisha kama walivyokuwa hapo zamani.


Kisha nikawawekea walinzi kwa kuwaarifu nikawaambia: Musikilize mulio wa baragamu. Lakini wao wakasema: Hatutausikiliza.


Wewe mwanadamu, nimekuweka kuwa mulinzi wa Waisraeli. Utakuwa ukisikiliza maneno ninayokuambia na kwenda kuwatolea maonyo yangu.


Basi, ewe mwanadamu, nimekuweka kuwa mulinzi wa Waisraeli. Utakaposikia neno kutoka kwangu utawapa onyo langu.


Wakati huo nitabadilisha luga ya watu, nitawawezesha kusema luga safi kusudi waniite mimi Yawe, na kuniabudu kwa moyo mumoja.


Siku hiyo, mimi Yawe nitawalinda wakaaji wa Yerusalema. Wanaokuwa wazaifu zaidi kati yao watakuwa na nguvu kama mufalme Daudi. Wazao wa Daudi watashika usukani kwa kuwaongoza watu wa Yuda kama Mungu, au kama malaika wa Yawe.


Wakati siku ya Pentekoste ilipotimia, wanafunzi walikuwa wamekusanyika wote pamoja wakibaki kwenye nafasi moja.


Kundi lote la waamini walikuwa na roho moja na nia moja. Hakuna hata mumoja wao aliyehesabia mali yake kuwa yake mwenyewe, lakini walishirikiana katika vitu vyote.


Wandugu zangu, ninawasihi ninyi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mukuwe na masikilizano kusudi matengano yasikuwe katikati yenu. Muishi katika umoja kabisa mukiwa na nia moja na wazo moja.


Kwa maana wakati wa sasa tunaona kama mwenye kuangalia ndani ya kioo kisichoonyesha wazi, lakini wakati utakaokuja tutaona waziwazi. Kwa sasa ninajua tu mambo machache, lakini nyuma nitajua kwa utimilifu kama vile Mungu anavyonijua mimi.


Mutii waongozi wenu na kushika maagizo yao. Kwa maana wao wanashugulika kila mara kwa ajili ya roho zenu, na wao wanapaswa kutoa habari ya kazi yao mbele ya Mungu. Kwa kufanya vile mutawaruhusu kufanya kazi yao kwa furaha wala si kwa huzuni, kwa maana haitawafalia kitu kama wakitumika katika huzuni.


Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!


Na wale wazee makumi mbili na wane na vile viumbe vine vya ajabu wakainama chini na kumwabudu Mungu, anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakisema: “Amina! Mungu asifiwe!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ