Halafu, Musa akamwambia Mungu: “Sasa, nikiwaendea Waisraeli na kuwaambia: ‘Mungu wa babu zenu amenituma kwenu’, nao wakiniuliza: ‘Jina lake ni nani?’, nitawaambia nini?”
Kwenda juu ya mulima murefu, ewe Sayuni, utangaze habari njema. Lalamika kwa nguvu, ewe Yerusalema, utangaze habari njema. Lalamika bila kuogopa. Uambie miji ya Yuda: Muangalie: Mungu wenu!
Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.
Utaletewa chakula na watu wa mataifa; wafalme watakupatia chakula bora. Hapo utatambua kwamba mimi Yawe ni Mwokozi wako; mimi Mwenye Nguvu wa Yakobo ni Mukombozi wako.
Wala hawatafundishana tena kila mutu na jirani yake, na kila mutu na ndugu yake na kusema “Mumujue Yawe”, kwa sababu wote, wadogo kama vile wakubwa, watanijua mimi Mungu. Maana nitawasamehe makosa yao, wala sitazikumbuka tena zambi zao.
Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe, wakati nitakapowatendea ninyi sio kulingana na mwenendo wenu na matendo yenu mabaya, lakini kwa heshima ya jina langu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.