Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 52:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Tena zamani ninyi watu wangu mulikimbilia Misri mukakaa kule. Halafu nyuma Waasuria waliwagandamiza bila sababu yoyote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 52:4
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walipeleka vilevile nyama na mali yao yote waliyokuwa wamechuma katika inchi ya Kanana, wakakwenda Misri. Yakobo aliwapeleka wazao wake wote:


wana wake, wajukuu wake wanaume na wanawake. Wote akawaleta Misri.


Yawe akamwambia Shetani: “Umemwona vizuri mutumishi wangu Yobu? Katika dunia hakuna mwingine anayekuwa kama yeye. Yeye ni mutu mukamilifu, wa usawa, mwenye kumwogopa Mungu na mwenye kuepukana na uovu. Yeye anadumu katika ukamilifu, ingawa wewe umenisukuma nimwangamize bure.”


Usimwache anayekutumainia kupata haya; lakini wafezeheke wote wanaokuasi kwa makusudi.


Umetufanya kama kondoo wanaopelekwa kuchinjwa; umetutawanya kati ya mataifa.


Ninaregea kwa ajili ya kulalamika, na koo langu limekauka. Macho yangu yamefifia, nikikungojea ewe Mungu wangu.


Nitauvunja uwezo wa Waasuria katika inchi yangu; nitawakanyagakanyaga katika milima yangu. Nitawaondolea watu wangu nira yao ya unyanganyi, na muzigo wa mateso yao.


Israeli ni kama kondoo wanaowindwa na kufukuzwa na simba. Kwanza waliangamizwa na mufalme wa Asuria, na sasa Nebukadneza mufalme wa Babeli, amevunjavunja mifupa yake.


Lakini wamefanya hivi kusudi maneno haya yaliyoandikwa katika Sheria yao yatimie: ‘Wamenichukia pasipo sababu.’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ