Na mara moja utakaposikia vishindo vya miguu kwenye vilele vya ile miforosadi, halafu, toka uende katika vita. Nitakuwa nimekwisha kukutangulia kuwapiga waaskari wa Wafilistini.”
Na hivi ndivyo mutakavyokula nyama yule: mutakuwa tayari kwa kusafiri, na kuvaa viatu na kuwa na fimbo zenu katika mikono. Tena mutamukula kwa haraka. Hiyo ni Pasaka ya Yawe.
Kwa sababu walikuwa wameondoka Misri kwa haraka, hawakuweza kutayarisha chakula cha safari, ila tu ule unga uliopondwa bila kutiwa chachu. Basi, wakapika mikate isiyotiwa chachu.
Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninaweka katika Sayuni jiwe la musingi, jiwe ambalo limeimarishwa. Jiwe la pembe, la bei kali, jiwe ambalo ni la musingi imara; jiwe linalokuwa na maandiko haya: Anayeamini hataanguka.
Nitawaongoza vipofu katika njia wasiyoifahamu, nitawaongoza katika njia ambazo hawazijui. Mbele yao nitaligeuza giza kuwa mwangaza, na pahali penye kuharibika patakuwa laini. Huo ndio mupango wangu wa kufanya, nami nitautimiza.
Hawatasikia tena njaa wala kuwa na kiu. Upepo wenye kuunguza wala jua havitawachoma, mimi niliyewahurumia nitawaongoza na kuwapeleka kwenye chemichemi za maji.
Mukifanya hivyo mutaonekana kama mwangaza wa mapambazuko, na mutapona haraka. Matendo yenu mema yatawatangulia, nami nitawalinda kutoka nyuma kwa utukufu wangu.
Yule atakayepasua njia atawatangulia, nanyi mutauvunja mulango wa muji na kutoka inje, mutapita na kutoka inje. Mufalme wenu, atawatangulia; Yawe mwenyewe atawatangulia.
Mwisho, wale waliokuwa chini ya bendera ya jeshi lililoongozwa na kabila la Dani, waliokuwa kama walinzi nyuma ya majeshi yote, wakasafiri, kundi moja nyuma ya lingine. Hawa waliongozwa na Ahiezeri mwana wa Amishadai.
Musikule sadaka hiyo na mikate iliyotiwa chachu. Kwa muda wa siku saba mutakula mikate isiyotiwa chachu, nayo ni mikate ya mateso – kwa sababu mulitoka Misri kwa haraka; kwa hiyo, muda wote mutakaoishi mutakumbuka ile siku mulipotoka Misri.
Wale watu wenye silaha wakawatangulia wale makuhani ambao walikuwa wanapiga mabaragumu, na walinzi wengine wakifuata nyuma ya Sanduku hilo, nayo mabaragumu yakilia kwa mufululizo.
Debora akamwambia Baraka: “Simama! Leo ni siku ambayo Yawe atamutia Sisera katika mikono yako. Yawe anakwenda mbele yako.” Basi, Baraka akashuka kutoka kwenye mulima Tabori akiwaongoza watu wake elfu kumi.